Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Yahaya Nawanda.
Na Mwandishi wetu-Mo Blog
MKUU
 wa wilaya ya Iramba mkoa wa Singida,Yahaya Nawanda, ameahidi kuishi kwa
 siku tano katika nyumba za kabila la kisukuma kijiji cha Kizonzo tarafa
 ya Shelui, ili kuhakikisha zoezi la kukusanya michango ya ujenzi wa 
zahanati ya kijiji hicho linafanikiwa.
Nawanda
 ametoa ahadi hiyo wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa 
uhamasishaji wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii 
(CHF),uliofanyika kwenye kijiji cha Kizonzo.
Alisema
 katika kipindi hicho atasimamia kwa karibu uchangiaji huo,ili ujenzi wa
 zahanati hiyo uweze kufanyika mapema iwezekanavyo.
“Ninyi
 ndugu zangu, mmekuwa mkipata taabu sana kufuata huduma ya afya kwenye 
zahanati ya kijiji cha Mgongo kwa kutembea umbali wa kilomita nane 
kwenda na kurudi. Akina mama wajawazito ndio wanaotaabika zaidi”, 
alifafanua Nawanda 
“Sasa
 tunasema hatutakubali kabisa ninyi muendelee kutaabika kufuata matibabu
 umbali mrefu kiasi hicho.Tunataka kipindi kifupi kijacho,matibabu 
muyapate hapa hapa kijijini kwenu”.
Kutokana
 na hali hiyo Nawanda amewataka wananchi kujiandaa mapema kwa zoezi hilo
 la uchangiaji wa ujenzi wa zahanati yao unaotarajiwa uanza mapema 
iwezekanavyo.
Kuhusu
 mfuko wa afya ya jamii (CHF),mkuu huyo wa wilaya,alisema suala la 
kujiunga na mfuko huo ni la lazima kwa madai kwamba afya bora ni mtaji 
wa mwili wa binadamu ye yote.
“Wilaya
 yetu ya Iramba, ni wilaya ya kwanza nchini kwa vituo vyake vyote vya 
afya kuwa na dawa za kutosha wakati wote.Kwa hiyo mwanachama wa CHF, 
nawahakikishia kuwa mtapata tiba wakati wote pindi watakapougua”,alisema
 DC huyo.
Kwa
 mujibu wa Dc Nawanda, kuku moja wa kienyeji mwenye thamani ya shilingi 
10,000 tu, anatosha kugharamia ada ya kaya moja yenye mume, mke moja na 
watoto wanane, kupata matibabu kwa kipindi cha mwaka moja bila kuongeza 
kiasi kingine cha fedha.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment