Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WIZARA ya Maji imetenga sh milioni 857 ili kukamilisha programu ya  
maji vijijini na usafi wa mazingira katika vijiji 10 vya Tarafa ya 
Kintinku  wilayani Manyoni, Singida vilivyopo kwenye mradi wa Benki ya 
Dunia.
  Fedha hizo zilizotengwa kwenye mwaka wa fedha 2014/2015 ni sehemu  ya 
sh bilioni 1.5 kwa ajili ya tarafa hiyo kuwawezesha wakazi wa vijiji 
hivyo  kuwa na uhakika wa majisafi na salama kabla ya mwisho wa mwaka 
2015.
  Naibu Waziri wa Maji, Amosi Makala, alitoa ahadi hiyo  alipozungumza 
na wakazi wa Kata ya Chikuyu, Tarafa ya Kintinku kuhusu  kumalizika kwa 
tatizo la maji lililowakabili kwa muda mrefu.
  Makala ambaye pia ni Mbunge wa Mvomero, alivitaja vijiji  
vitakavyonufaika na mradi huo kuwa ni Kintinku, Lusilile, Ngaiti, Mvumi,
  Maweni, Chilejeho, Mtiwe, Chikuyu, Mwiboo na Mbwasa.
  Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa tarafa hiyo, Diwani wa Viti  
Maalumu, Zinduna Abdallah (CCM), alimweleza naibu waziri huyo kwamba 
tatizo la  maji limeharibu ndoa za watu.
  Mhandisi wa Sekretarieti ya mkoa huo, Yunusi Rugeyamu, alisema sensa  
ya watu na makazi ya mwaka 2012 inaonyesha kuwa Singida ilikuwa na 
wakazi  1,370,637 na kwamba hadi Desemba mwaka jana wakazi 656,932 
waishio vijijini  wanapata maji.
Chanzo;Tanzania Daima   
0 comments:
Post a Comment