Home » » ABIRIA WA TRENI WAKWAMA MANYONI

ABIRIA WA TRENI WAKWAMA MANYONI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

ZAIDI ya abiria 700 waliokuwa wakisafiri na treni ya abiria wakitokea Kigoma kuelekea Dar es Salaam, wamekwama kwa siku mbili wilayani Manyoni, baada ya treni ya mizigo kuanguka.
Wakizungumza na waandishi wa habari waliofika eneo hilo jana, abiria hao wamelilalamikia Shirika la Reli kutokana na kutokuwa na utaratibu mzuri wa kusafirisha abiria wake pindi tatizo linapojitokeza.
Walisema walipofika Manyoni majira ya mchana, walielezwa kuwa treni ya mizigo ilikuwa imeanguka kituo kinachofuatia cha Saranda, hivyo wasubiri utaratibu.
“Lakini cha kushangaza mabasi ambayo yalikuwa yakiletwa na Shirika la TRL yalikuwa machache kwa sababu abiria tulikuwa wengi,” alisema mmoja wa abiria hao, Anton Beni.
Walisema kutokana na hali hiyo walilazimika kulala nje huku wakiwa na watoto wadogo na wengine wagonjwa, kwani mabasi yalipokuwa yakifika kuwachukua hakukuwa na utaratibu na kusababisha watu kugombea na kusema hadi sasa baadhi ya abiria hawajui hatima yao ya kufika Dar es Salaam.
Meneja wa Kanda wa TRL kutoka Dar es Salaam, Philipo Rutizibwa, alisema suala la abiria waliokwama Manyoni wameshafanya utarabu wa mabasi na yameshaanza kuwachukua kuwapeleka wanakokwenda
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa