Mkuu
 wa Mkoa wa Singida Mheshimiwa Mhandisi Mathew John Mtigumwe amemtaka 
Mkuu wa Wilaya ya Singida kusimamia utekelezaji wa maamuzi ya kuhamishia
 makao makuu ya halmashauri ya Singida katika mji mdogo wa Ilongero 
ndani ya kipindi cha miezi sita  ili kusogeza huduma karibu na wananchi 
wa halmashauri hiyo.
Mheshimiwa
 Mhandisi Mtigumwe amefikia uamuzi huo kutokana na taarifa za kuwepo 
watu wachache wanaotaka kufanya mabadiliko ya makao makuu bila ya 
kusikiliza mawazo ya wananchi wengi huku wananchi wakipendelea makao 
makuu ya halmashauri hiyo kuwa katika mji mdogo wa Ilongero.
Ameongeza
 kuwa baraza la madiwani la halmashauri ya Singida linapaswa kuketi tena
 na kufanya maamuzi sahihi kwa maslahi ya wananchi wengi huku akiongeza 
kuwa endapo wanataka kufanya mabadiliko wayafanye wakiwa tayari 
wameshahamia katika halmashauri yao tofauti na sasa ambapo bado ofisi 
zipo manispaa ya Singida.
Mheshimiwa
 Mhandisi Mtigumwe amesema wananchi wanataka kupatiwa huduma kwa ukaribu
 hivyo halmashauri kuhamishiwa Ilongero itasaidia kusogeza Huduma ambapo
 zitatolewa kwa ufanisi huku akimshauri Mkurugenzi wa halmashauri hiyo 
kujipanga ndani ya kipindi hicho waanze kutumia ofisi chache zilizopo.
Aidha
 Mheshimiwa Mhandisi Mtigumwe amewataka wananchi wa halmashauri na Mkoa 
mzima wa Singida kujituma na kufanya kazi kwa bidii, wakulima wajiandae 
FEMA kwa msimu huu wa kilimo na kujitahidi kutunza vyakula ili 
kujiepusha na njaa na wafanyabiashara watumie fursa mbalimbali 
kujiongezea kipato.
Naye
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida Martha Mlata 
amesema chama hicho mkono mapendekezo ya wananchi yakutaka makao makuu 
kuwa katika mji mdogo wa Ilongero na kuahidi kufuatilia na kusimamia 
utekelezaji wake.
Katika
 kuunga mkono mapendekezo ya wananchi Mbunge wa jumbo la Singida 
kaskazini la kaskazini Mhe. Lazaro Nyalandu amesema kufikia mwezi 
Januari ataweka ofisi za Mbunge katika mji wa  I'll wananchi wapate 
Huduma na kumfikishia kero kwa ukaribu zaidi.
0 comments:
Post a Comment