Home » » MKUU WA MKOA AELEKEZA HALMASHAURI YA SINGIDA KUHAMIA ILONGERO NDANI YA KIPINDI CHA MIEZI SITA

MKUU WA MKOA AELEKEZA HALMASHAURI YA SINGIDA KUHAMIA ILONGERO NDANI YA KIPINDI CHA MIEZI SITA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mkuu wa Mkoa wa Singida Mheshimiwa Mhandisi Mathew John Mtigumwe amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Singida kusimamia utekelezaji wa maamuzi ya kuhamishia makao makuu ya halmashauri ya Singida katika mji mdogo wa Ilongero ndani ya kipindi cha miezi sita  ili kusogeza huduma karibu na wananchi wa halmashauri hiyo.
Mheshimiwa Mhandisi Mtigumwe amefikia uamuzi huo kutokana na taarifa za kuwepo watu wachache wanaotaka kufanya mabadiliko ya makao makuu bila ya kusikiliza mawazo ya wananchi wengi huku wananchi wakipendelea makao makuu ya halmashauri hiyo kuwa katika mji mdogo wa Ilongero.
Ameongeza kuwa baraza la madiwani la halmashauri ya Singida linapaswa kuketi tena na kufanya maamuzi sahihi kwa maslahi ya wananchi wengi huku akiongeza kuwa endapo wanataka kufanya mabadiliko wayafanye wakiwa tayari wameshahamia katika halmashauri yao tofauti na sasa ambapo bado ofisi zipo manispaa ya Singida.
Mheshimiwa Mhandisi Mtigumwe amesema wananchi wanataka kupatiwa huduma kwa ukaribu hivyo halmashauri kuhamishiwa Ilongero itasaidia kusogeza Huduma ambapo zitatolewa kwa ufanisi huku akimshauri Mkurugenzi wa halmashauri hiyo kujipanga ndani ya kipindi hicho waanze kutumia ofisi chache zilizopo.
Aidha Mheshimiwa Mhandisi Mtigumwe amewataka wananchi wa halmashauri na Mkoa mzima wa Singida kujituma na kufanya kazi kwa bidii, wakulima wajiandae FEMA kwa msimu huu wa kilimo na kujitahidi kutunza vyakula ili kujiepusha na njaa na wafanyabiashara watumie fursa mbalimbali kujiongezea kipato.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida Martha Mlata amesema chama hicho mkono mapendekezo ya wananchi yakutaka makao makuu kuwa katika mji mdogo wa Ilongero na kuahidi kufuatilia na kusimamia utekelezaji wake.
Katika kuunga mkono mapendekezo ya wananchi Mbunge wa jumbo la Singida kaskazini la kaskazini Mhe. Lazaro Nyalandu amesema kufikia mwezi Januari ataweka ofisi za Mbunge katika mji wa  I'll wananchi wapate Huduma na kumfikishia kero kwa ukaribu zaidi.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa