Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Daktari bingwa wa macho Mkoani Singida Ngh'ungu Kuzenza 
akimfanyia uchnguzi wa macho mgonjwa wa kisukari katika kuadhimisha siku
 ya kisukari duniani. 
Na Grace Singida
Wagonjwa
 wa kisukari Mkoani Singida leo wamefanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya 
macho na daktari bingwa wa macho katika kuadhimisha siku ya ugonjwa wa 
kisukari duniani ikiwa na kauli mbiu ya ugonjwa wa kisukari na magonjwa 
ya macho.
Mganga
 Mfawidhi wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Singida Dokta Ramadhani 
Kabala amewaambia wagonjwa wa kisukari waliohudhuria kufanyiwa uchunguzi
 wa macho kuwa maadhimisho hayo mwaka huu yamelenga kuzuia wagonjwa 
wasiathirike zaidi na magonjwa yatokanayo kisukari.
Dokta
 Kabala amesema ugonjwa wa kisukari hushambulia zaidi macho, figo na 
moyo hivyo serikali imeweka mkazo wa kuwafanyia uchunguzi ili kubaini 
tatizo ili wapatiwe matibabu mapema au kuzuia yasitokee kabisa kwa 
kufuata kanuni na taratibu za ugonjwa huo.
Ameongeza
 kuwa ugonjwa wa kisukari unawakumbusha watu kuishi kwa kufuata kanuni 
bora za afya kama kula mlo kamili, kula matunda badala ya juisi 
zilizotengenezwa viwandani, kufanya mazoezi na kupunguza vilevi na 
sigara hivyo wagonjwa wa kisukari hawana togauti na watu wengine 
isipokuwa wao hushauriwa kufuata kanuni hizo kwa umakini mkubwa.
Dokta
 Kabala amewakumbusha kutumia dawa kwa kufuata usahuri wa daktari wao 
pamoja na kuhudhuria kliniki za kisukari kwakuwa kliniki hizo 
zinawasaidia katika kushauriana namna bora ya kuishi kwa kufuata 
masharti wananyopewa pamoja kuelimishanzaidi juu ya ugonjwa huo.
Naye
 Daktari bongwa wa macho Mkoani Singida Dokta Ngh’ungu Kuzenza amesema 
utaratibu huo unasaidia kuzuia au kupunguza madhara ya ugonjwa wa 
kisukari kwakuwa wengi watatambuliwa kabla hawajafikia hatua ya 
kupofuka.
Dokta
 Kuzenza ameongeza kuwa changamoto kubwa ni watu wengi kutopima ugonjwa 
wa kisukari mapema mpaka wanapougua na hivyo kujikuta wameshaathirika 
macho ndipo hutafuta huduma.
Kwa
 upande wake mmoja kati ya wagonjwa wa kisukari 76 waliopata huduma ya 
kibingwa ya macho Bi Asha Selemani Waziri Mkazi wa Iguguno ameema 
serikali imeweka utaratibu mzuri wa kuwapima macho ili waweze kupata 
tiba mapema.
Bi
 Waziri ameiomba serikali kuendelea kuweka utaratibu wa kuwapima 
wagonjwa wa kisukari magonjwa mbalimbali kama moyo na figo huku 
akiwashauri wagonjwa wa kisukari kufuata ushauri wanaopewa na  wataalamu wa afya.
0 comments:
Post a Comment