Na. Lilian Lundo – MAELEZO
Dar es Salaam
28.11.2016
IMEELEZWA
 kuwa Uongozi bora na matumizi bora katika usimamizi wa fedha za 
Serikali ni miongoni mwa sababu zilizoiletea Tanzania maendeleo tangu 
ilipopata uhuru mwaka 1961.
Hayo
 yamebainishwa leo Jijini Dar es Salaam na Spika Mstaafu, Pius Msekwa 
wakati wa mahojiano maalum na mwandishi wa habari hii kuhusiana na hatua
 ambazo Tanzania imepiga tangu ipate uhuru mwaka 1961.
Msekwa
 alisema kuwa uongozi bora pamoja matumizi bora ya fedha ndizo nguzo kuu
 zilizoiletea Tanzania maendeleo yanayoonekana leo ambapo takribani 
sekta zote zimepiga hatua kubwa ukilinganisha na kipindi cha uhuru mwaka
 1961. 
“Wakati
 tunapata uhuru mwaka 1961 tulirithi vitu vichache kutoka kwa wakoloni 
ambavyo ni shule hospitali ya Muhimbili iliyokuwa ikijulikana kama 
Princess Magreth ambayo kwa sasa imepiga hatua na kuweza kufanya 
upasuaji wa moyo ambao haukuwahi kufanyika kwa miaka ya nyuma,” 
alifafanua Msekwa.
Alisema
 kuwa maendeleo yote hayo yametoka na juhudi za marais waliopita na 
aliyepo, katika uongozi wao ambapo wamekuwa wakipambana na maadui watatu
 wa maendeleo ambao ni ujinga, maradhi na umasikini.
Aidha
 alisema kuwa viongozi hao wamekuwa wakipambana na maadui hao kulingana 
na fedha ambazo zimekuwa zikipatikana katika kipindi cha uongozi wao.
Msekwa
 aliwataka Watanzania kuendelea kumuenzi Mwalimu Julius Kambarage 
Nyerere kutokana na misingi aliyoiacha ambayo imeweza kutumiwa na 
viongozi wa nchi na kuendelea kuleta maendeleo ambayo Tanzania 
inajivunia hadi sasa.
0 comments:
Post a Comment