Na Eleuteri Mangi- MAELEZO, Dodoma
Maeneo
 ya Kititimo na Kisaki mkoani Singida yametajwa kuwa ni miongoni mwa 
maeneo mazuri nchini yenye uwezo wa kuzalisha umeme kwa kutumia nguvu ya
 upepo.   
Naibu
 Waziri wa Nishati na Madini Medard Kalemani amesemwa hayo leo Bungeni 
mjini Dodoma alipokuwa akijibu sawali la Mbunge wa Viti Maalum Jesca 
Kishoa lililohoji ni lini mradi huo utaanza kuzalisha umeme huo mkoani 
humo.
Akijibu
 swali hilo Naibu Waziri Kalemani amesema Serikali kwa kushirikiana na 
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imekuwa ikifanya tafti kwa ajili ya 
kuzalisha umeme kwa kutumia upepo katika maeneo mbalimbali nchini.
“Ujenzi
 wa mradi wa uzalishaji wa umeme wa upepo utaanza ifikapo Aprili 2017 na
 kutarajiwa kukamilika mwaka 2019 baada ya majadiliano kati ya TANESCO 
na kampuni ya Wind East Africa Ltd kukamilika mwezi Desemba 2016” 
amesema Naibu Waziri Kalemani.
Kupitia
 tafiti hizo, Naibu Waziri Kalemani amesema kuwa kampuni binafsi ya Wind
 East Africa Ltd yenye Wabia watatu ambao ni Six Telecoms (Tanzania), 
kampuni ya Kimataifa ya Aldwych ya nchini Uingereza pamoja na moja ya 
wajumbe wa Benki ya Dunia (IFC) ambao utagharimu jumla ya kiasi cha Dola
 za Kimarekani milioni 264.77.
Aidha,
 Naibu Waziri Kalemani kampuni nyingine inayoonesha nia ya kuwekeza 
katika mradi wa kufua umeme wa upepo ni mkoani Singida kuwa ni Geowind 
Ltd ambayo ipo tayari kuzalisha umeme wa Megawati 50 eneo la Kititimo 
ambapo kampuni hiyo tayari ina eneo la hekta 1,450, mradi huo 
unatarajiwa kugharimu Dola za Kimarekani milioni 136 na kukamilika mwaka
 2018. 

0 comments:
Post a Comment