Home » » MKAZI WA SINGIDA JELA MIAKA 30 BAADA YA KUKIRI KULAWITI MVULANA WA MIAKA 9.

MKAZI WA SINGIDA JELA MIAKA 30 BAADA YA KUKIRI KULAWITI MVULANA WA MIAKA 9.


Bango la mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida.Picha  na Nathaniel Limu.
Na Nathaniel Limu.
Kijana mkulima wa kijiji cha Ihanja jimbo la Singida Magharibi Samwel Simon (22) amehukumiwa kutumikia jela miaka 30 baada ya kukiri kosa la kumlawiti kijana wa kiume mwenye umri wa miaka tisa (jina tunalo).
Mvulana huyo mdogo ni mkazi wa kijiji cha Nkhoiree tarafa ya Ihanja jimbo la Singida Magharibi.
Awali mwendesha mashitaka inspekta msaidizi wa polisi Shukurani Magafu, alidai mbele ya hakimu wa mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida Terrysophia Tesha kuwa mnamo juni 12 mwaka huu katika muda ambao haujafahamika, mshitakiwa Samwel alimlawiti mvulana huyo mdogo na kumsababishia maumivu makali katika sehemu yake ya kutolea haja kubwa.
Magafu amesema siku ya tukio, mshitakiwa alimlaghai kijana huyo wa kiume na kisha kuingia naye ndani ya chumba chake cha kulala na baada ya kumvua kaptura, alimkaba kwa nguvu na kuanza  kumwingilia kinyume na maumbile.
Amesema wakati mshitakiwa akiendelea na unyama wake, kijana huyo alikuwa akipiga kelele ambazo zilichangia majirani na watu waliokuwa karibu na eneo la tukio kufika haraka kwa lengo la kujua kinachomsibu kijana huyo.
“Watu walipofika eneo la tukio, walimkuta mshitakiwa bado anaendelea kuvaa suruali yake na ndipo walipomkamata na kumfunga kwa kamba ya katani inayotumika  kufungia ng’ombe na kumpeleka kituo kidogo cha polisi Ihanja”, alisema mwendesha mashitaka huyo.
Amesema mshitakiwa alipofikishwa kituo cha polisi Ihanja, bila kusumbua, alinyoosha maelezo na kukiri kuwa ni kweli amemwingilia kimwili kinyume na maumbile kijana huyo wa kiume.
Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, mwendesha mashitaka Magafu alisema pamoja na mshitakiwa kutokuwa na rekodi yo yote ya makosa ya uhalifu,l akini kitendo alichomfanyia mtoto huyo mdogo hakivumiliki mbele ya jamii.
Kwa upande wake mshitakiwa, aliiomba mahakama hiyo imwonee huruma na kumwachia huru kwa vile amefanya kosa hilo kwa kusukumwa na pombe nyingi aliyokuwa ameitumia siku hiyona pia hajaisumbua mahakama na hilo ni kosa lake la kwanza toka a
Habari kwa hisani ya MO BLOG

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa