Home » » Mtoto Wa Afrika Ilivyokuwa Singida

Mtoto Wa Afrika Ilivyokuwa Singida

Watoto wa Kompasheni, Kanisa la Moravian Singida Mjini wakifuatilia moja ya tukio, maadhimisho ya mtoto wa Afrika,
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Tumaini, Mjini Singida iliyo maalumu kwa wasiosikia, wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi
Mkurugenzi wa Manispaa Singida, Mathias Mwangu(katikati), Afisa maendeleo jamii, Daffi Imanuel(kushoto), na mmoja wa ofisa kati
 Wanafunzi wa Shule ya Msingi Tumaini, Mjini Singida iliyo maalumu kwa wasiosikia, wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi

Na Elisante John, Singida
Juni 17, 2012:ZAIDI ya watoto 2,900 wanaishi mazingira hatarishi Manispaa ya Singida, hivyo kuchochea vitendo viovu, kwa kukosa malezi bora.
 
Hali inayosababishwa na watoto wengi kukosa msingi imara wa malezi, wakati wote wa makuzi yao.
 
Kati ya watoto hao Wasichana ni 1,454 na wavulana 1,472 ambao baadhi yao hulazimika kujiigiza katika kwenye vitendo viovu, ili kujikimu maisha ya kila siku.
 
Mkurugenzi wa Manispaa Singida, Mathias Mwangu, amesema hayo kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika, yaliyofanyika juzi, katika viwanja vya Utamaduni, mjini Singida.
 
Mwangu amesema, licha ya watoto hao kujihusisha na tabia hizo mbaya katika jamii, pia wanalazimika kukosa haki za msingi, kama vile elimu, huduma za afya, chakula na malazi bora.
 
Amesema, Manispaa yake kwa kushirikiana na wadau wake, inaangalia uwezekano kuandaa utaratibu maalumu, utakaowezesha watoto hao kuungana na familia zao, kwa faida yao na Taifa kwa ujumla.
 
Siku ya mtoto wa Afrika huadhimishwa Juni 16 kila mwaka, kukumbuka mauaji ya Soweto,nchini Afrika Kusini, wakati wakidai elimu bora; Kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘Haki ya watoto walemavu ni jukumu letu kuzilinda,kuziheshimu, kuzidumisha na kuzitimiza’

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa