Mfanyabiashara ajiua kwa risasi, mwingine achinjwa
Watu wawili wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti yaliyotokea mkoani Singida mwishoni mwa wiki likiwemo la mfanyabiashara kujipiga risasi kichwani na mwingine huchinjwa shingo, kutolewa koromeo na ulimi.
Padri anayedaiwa kutelekeza mtoto kuburuzwa kortini tena leo
Mahakama
 ya Mwanzo Utemini iliyopi mjini hapa Mkoa wa Singida, leo inatarajia 
kuendelea kusikiliza kesi inayomkabili Padri  wa Kanisa Katoliki mjini 
hapa,  Deogratius Makuri ya kumtelekeza bila  kumhudumia mtoto wake wa 
kike aliyedaiwa kuzaa na muumini wake.
Kesi hiyo ilisikilizwa wiki iliyopita na kuahirishwa baada ya kudaiwa mahakamani hapo kuwa padri huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi wa muda mrefu na Maria Boniphance (26) aliyekuwa mhudumu wa kanisa hilo Parokia ya Singida mjini.
Ilidaiwa mbele ya hakimu wa mahakama hiyo, Ferdnand Njau kuwa wakati wote huo wa mahusiano ya kimapenzi, ndipo mshitakiwa alimpa ujauzito na kuzaa naye mtoto wa kike.
Mlalamikaji (Maria) alidai mahakamani hapo kuwa baada ya ujauzito huo, aliamua kulifikisha suala hilo kwa wazazi wake ambao walimwendea padri huyo na kukubali kuhusika na mimba hiyo.
Alidai kuwa padri huyo aliahidi kwa maandishi kuwa atamtunza mtoto wake (jina tunalo) hadi hapo atakapokuwa na uwezo wa kujitegemea, kinyume chake ahadi hiyo alitekeleza kwa miezi michache na akasitisha matunzo.
"Pamoja na kuchukua hatua mbalimbali ikiwamo kufikisha suala hilo ofisi ya ustawi wa jamii... aliahidi kupitia hati ya mkataba kuwa atakuwa anatoa kila mwezi Sh. 80,000 na akishindwa afikishwe mahakamani, ndiyo mimi nimeamua kumshitaki, ”alidai mlalamikaji huyo.
Ilidaiwa kuwa pamoja na ahadi hiyo padri Makuri alianza kutoa madai mbalimbali kwamba mtoto huyo siyo wake wa kuzaa, na hapo ndipo aliamua kusitisha matunzo kama alivyoahidi. .
 
Kesi hiyo ilisikilizwa wiki iliyopita na kuahirishwa baada ya kudaiwa mahakamani hapo kuwa padri huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi wa muda mrefu na Maria Boniphance (26) aliyekuwa mhudumu wa kanisa hilo Parokia ya Singida mjini.
Ilidaiwa mbele ya hakimu wa mahakama hiyo, Ferdnand Njau kuwa wakati wote huo wa mahusiano ya kimapenzi, ndipo mshitakiwa alimpa ujauzito na kuzaa naye mtoto wa kike.
Mlalamikaji (Maria) alidai mahakamani hapo kuwa baada ya ujauzito huo, aliamua kulifikisha suala hilo kwa wazazi wake ambao walimwendea padri huyo na kukubali kuhusika na mimba hiyo.
Alidai kuwa padri huyo aliahidi kwa maandishi kuwa atamtunza mtoto wake (jina tunalo) hadi hapo atakapokuwa na uwezo wa kujitegemea, kinyume chake ahadi hiyo alitekeleza kwa miezi michache na akasitisha matunzo.
"Pamoja na kuchukua hatua mbalimbali ikiwamo kufikisha suala hilo ofisi ya ustawi wa jamii... aliahidi kupitia hati ya mkataba kuwa atakuwa anatoa kila mwezi Sh. 80,000 na akishindwa afikishwe mahakamani, ndiyo mimi nimeamua kumshitaki, ”alidai mlalamikaji huyo.
Ilidaiwa kuwa pamoja na ahadi hiyo padri Makuri alianza kutoa madai mbalimbali kwamba mtoto huyo siyo wake wa kuzaa, na hapo ndipo aliamua kusitisha matunzo kama alivyoahidi. .
					CHANZO:
					NIPASHE
				
Ikungi kutumia bil. 25/-
 
 
 
 
 HALMASHAURI ya Wilaya ya Ikungi  mkoani Singida, inatarajia kutumia 
shilingi bilioni 25.696 katika mwaka wa  fedha 2014/2015 kwa ajili ya 
matumizi ya kawaida na shughuli za maendeleo.
  Akisoma taarifa ya bajeti kwenye  kikao maalumu cha Baraza la Madiwani
 wa halmashauri hiyo jana, Makamu  Mwenyekiti Ally Nkangaa, alisema 
katika kipindi hicho kiasi cha sh bilioni  15.426 ni kwa ajili ya 
mishahara ya watumishi wake.
  Hata hivyo alisema katika bajeti  iliyopita halmashauri iliomba 
kuidhinisha kiasi cha shilingi bilioni 16.953  ambapo hadi kufikia mwezi
 Desemba mwaka huu, jumla ya shilingi milioni 512.322  zilikuwa 
zimetumika kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo.
  Nkhangaa alisema katika utekelezaji  wa bajeti, zipo changamoto 
mbalimbali ambazo ni pamoja na baadhi ya vijiji na  kata kutochangia 
nguvu kazi na fedha.
Chanzo;Tanzania Dama 
Mvua kubwa zaleta madhara Singida, watu watano wahofiwa kufa maji
Kamanda
 wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida, SACP Geofrey Kamwela, akizungumza 
na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na tukio la maafa ya 
mvua kubwa iliyosababisha vifo.
Na Nathaniel Limu, Singida 
MVUA
 kubwa zilizoanza kunyesha mkoani Singida zimeanza kuleta maafa baada ya
 watu watano kuhofiwa kufa maji kutokana na gari waliolokuwa wakisafiria
 kusombwa na maji ya mto.
 Kamanda
 wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, SACP Geofrey Kamwela amesema tukio 
hilo limetokea Desemba saba mwaka huu saa 3:30 asubuhi huko katika mto 
wa Nzalala kijiji cha Kisimba tarafa ya Kisiriri wilayani Iramba.
Amesema
 siku ya tukio, abiria 16 waliokuwa wakitoka kijiji cha Doromoni kwa 
kutumia Landrover 110 TDI lenye namba za usajili T.499 ATR, lilisombwa 
na maji ya mto wakati dereva wake akijaribu kuvuka mto Nzalala.
 Akifafanua,
 amesema walimpofika kwenye mto huo abiria hao walimwomba dereva huyo 
asubiri maji ya mto yapungue ili waweze kuvuka lakini dereva huyo 
alikataa kwa madai maji ni machache.
 “Wakati
 gari hilo lilipofika katikati ya mto, lilizimika ghafla na wakati huo 
huo maji ya mto yaliongezeka na kulifunika gari.  Dereva na kondakta 
waliweza kufanikiwa kutoka na kukimbilia kusikojulikana”
 Aidha,
 amesema abiria 11 waliweza kuokolewa na wamelazwa katika hospitali ya 
wilaya ya Iramba na watano hadi sasa haijulikani iwapo wamekufa ndani ya
 landrover au wamesomba na maji na kupelekwa kusikojulikana.
 Katika
 hatua nyingine, Kamanda Kamwela, ametoa wito kwa madereva wa vyomba vya
 moto, baiskeli na watembea kwa miguu kuchukua tahadhari wakati wa 
kuvuka mito au mabonde kipindi hiki cha mvua kubwa zinazoendelea 
kunyesha.
 Alitumia
 fursa hiyo kushauri mamlaka zinazohusika kutengeneza madaraja kwenye 
mito au mabonde badala ya kuweka zege ambalo husaidia tu katika kipindi 
cha kiangazi.
 “Aidha nashauri abiria nao wasikubali kujazwa kwenye vyombo vya usafiri tofauti na uwezo hali wa gari” amesema.
Na Mo Blog 
MAJAMBAZI WAWILI WAUAWA MKOANI SINGIDA.
TUNAOMBA RADHI KWA HII PICHA
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela,akionyesha bunduki ya kijeshi aina ya SMG no.34555 iliyokuwa ikitumiwa na watu wawili wanaodhaniwa kuwa majamabazi katika kijiji cha Manga manispaa ya Singida.
WATU 
wawili wakazi wa manispaa ya Singida ambao majina yao bado 
hayajajulikana,wakiwa kwenye Jokofu la kuhifadhia maiti baada ya kuuawa 
wakati wa majibishano ya risasi na polisi.
JESHI  la Polisi mkoani Singida limewauwa watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakati wa kurushiana rasasi.
Kamanda
 wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, SACP, Geofrey Kamwela amesema tukio 
hilo limetokea desemba tisa mwaka huu saa 12:00 jioni, huko katika 
kijiji cha Manga nje kidogo ya mji wa Singida.
Amesema
 watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wakiwa na bunduki moja ya 
kijeshi aina ya SMG, walifika kijijini hapo kwa lengo la kufanya 
uhalifu.
Kamanda
 Kamwela, amesema watu hao ambao miili yao imehifadhi kwenye chumba cha 
mochwari katika hospitali ya mkoa, majina na makazi yao bado 
hayajajulikana.
Akifafanua,
 amesema taarifa za siri kutoka kwa raia wema zilifikia jeshi la polisi 
na ndipo askari polisi walipofika kwenye eneo la tukio.
“Baada
 ya polisi kufika kijijini hapo watu hao walistuka kuwa wanafuatilwa na 
askari polisi na hivyo kuanza kukimbia kuelekea kijiji cha Uhamaka kwa 
kutumia pikipiki yenye namba za usajili T. 634 BTW aina ya Sanlag yenye 
rangi nyeusi”,amesema Kamwela.
Amesema walipoona Polisi wanawakaribia waliamua kutelekeza pikipiki yao hiyo na kuanza kukimbilia porini kwa miguu.
“Hali
 ilipokuwa ngumu zaidi, walianza kuwarushia polisi risasi, hivyo polisi 
nao ikwabidi kujibu mapigo.  Katika majibizao hayo ya risasi, majambazi 
mawili yaliweza kujeruhiwa huku mmoja akifanikiwa kutoroka”
Amesema
 majambazi hayo yaliyojeruhiwa yalifariki dunia wakati yanakimbizwa 
katika hospitali ya mkoa kwa matibabu,lakini yakafia njiani.
Amesema katika eneo la tukio, ilipatikana 
bunduki
 moja aina ya SMG yenye namba 34555 ikiwa na risasi saba kwenye 
magazine.  Pia pikipiki iliyokuwa iantumiwa na majambazi hayo, iliwezea 
kupatikana.
Kamwela
 alitoa wito kwamba wananchi waendelee na moyo huo huo wa kuwafichua 
watu wanaowatilia shaka ili waweze kudhibitiwa mapema kabla ya kufanya 
uhalifu.
Kwa hisani ya Mtandao wa Singida Yetu 
WATANO WAFA MAJI NA WENGINE 11 WANUSURIKA
WATU
 watano wanahofiwa kufa maji na wengine 11 wamenusurika, baada  ya  gari
 waliyokuwa wakisafiria  kusombwa na maji  ya mto  kufuatia mvua kubwa 
zinazoendelea kunyesha mkoani mkoani Singida.
Kwa
  mujibu wa Kamanda wa Polisi  mkoa wa Singida Kamishina msaidizi 
mwandamizi  Geofrey Kamwela,  tukio hilo limetokea jana  majira ya  saa 
3: 30 asubuhi katika Kijiji cha Kisimba Wilayani Iramba.
 Amesema  watu hao waliokuwa wakisafiri kwa gari yenye namba za usajili 
T.499 ATR aina ya Land rover 110 TDI,  walikuwa wakijaribu kuvuka  mto  
Nzalala kutoka   eneo Doromoni kwenda Kiomboi Mjini.
Kamanda
 Kamwela amesema wakati dereva  ambaye hajatambuliwa jina wala makazi 
akijaribu kuvusha, gari hiyo ilizimika  katikati ya mto kabla ya 
kosombwa na  maji ikiwa na abiria 16 ndani.
Amesema
 abiria 11 kati yao wameokolewa na kupelekwa hospitali  ya Wilaya ya  
Iramba kwa matibabu, wakati juhudi za  kufukua gari hiyo iliyofukiwa kwa
 mchanga  mita chache kutoka eneo la  tukio na kutafuta watu wengine 
watano ambao hawajulikani walipo zinaendelea kufanywa.
Dereva   wa gari hiyo na   kondakta wake wanasadikiwa kutoweka baada  ya  tukio hilo na polisi wanaendelea kuwasaka.
Ajali yaua watano
Singida.Abiria watano wamekufa baada ya gari 
aina ya Landrover 110 waliyokuwa wanasafiria kusombwa na maji katika 
Kijiji cha Doromoni Wilaya ya Iramba.
Katika ajali hiyo iliyotolea jana, watu wengine 11 walinusurika baada ya kuruka na kuogelea mara baada ya gari hiyo kupinduka.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo.
Kamwela alisema ajali hiyo ilitokea majira ya 
asubuhi wakati gari hilo likiwa linabeba abiria 16 kutoka Kijiji cha 
Doromoni wilayani Iramba kuelekea Kiomboi mjini.
Alisema chanzo cha ajali hiyo ni kujaa kwa maji katika Mto Nzalala kiasi cha kulifunika daraja.
Kamwela alisema wakati dereva alipojaribu kuvuka, gari hiyo ilizidiwa nguvu na maji, hivyo kuisomba.
Baadhi ya abiria walionusurika kwenye ajali hiyo 
walisema kwamba walipofika kwenye daraja hilo walimwambia dereva 
asivuke, bali asubiri maji yapungue.
Walidai dereva alikaidi agizo hilo na kuamua 
kuvuka na alipofika katikati alionekana kubabaika na maji kabla ya maji 
kuizidi nguvu gari.
Habari ambazo pia hazijathibitishwa zilidai kuwa dereva na kondakta wa gari hilo waliruka na kukimbia eneo la ajali.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
Polisi yaua majambazi wawili
JESHI la Polisi mkoani Singida limewaua kwa kuwapiga  risasi 
majambazi wawili waliokuwa wakijiandaa kufanya uhalifu katika Kijiji cha
  Manga nje kidogo ya mji wa Singida.
  Kamanda wa Polisi mkoani Singida, Godfrey Kamwela  alisema tukio hilo 
limetokea juzi, saa 12:00 jioni baada ya polisi kupata  taarifa za siri 
kutoka kwa raia wema.
  Kamwela alisema majambazi hayo yalikuwa na bunduki moja  aina ya SMG 
yenye namba 34555 ikiwa na risasi saba kwenye magazine, huku wakitumia  
pikipiki T 634 BTW Sanlg.
  Aidha, Kamanda Kamwela alisema askari polisi walifika  katika eneo 
hilo, na watu hao walistuka kwa kuwa wanafuatiliwa na askari na  hivyo 
kuanza kukimbia kuelekea Kijiji cha Uhamaka kwa kutumia pikipiki hiyo.
  Hata hivyo, alisema walipoona polisi wanawakaribia  waliitelekeza 
pikipiki hiyo na kuanza kukimbia porini kwa miguu, lakini hali  
ilipokuwa ngumu zaidi walianza kuwarushia polisi risasi, hivyo polisi 
nao  walilazimika kujibu.
  “Majibizano hayo ya risasi yalipelekea majambazi wawili  kujeruhiwa 
huku mmoja akifanikiwa kukimbia. Majeruhi hao walifariki dunia  wakati 
wakikimbizwa hospitali ya mkoa kwa matibabu. Maiti zimehifadhiwa  
hospitalini hapo kwa ajili ya kutambuliwa na ndugu zao,” alisema 
Kamwela.
  Alisema kwenye eneo la tukio ilipatikana bunduki moja  aina ya SMG 
ikiwa na risasi saba na pikipiki iliyokuwa wakiitumia kukimbia.  Polisi 
wanaendelea na uchunguzi   ili  kubaini kama kuna mtandao wa majambazi 
pamoja na kumsaka mtuhumiwa aliyekimbia.
  Wakati huohuo, polisi mkoani hapa inawashikilia watu  wanne akiwemo 
mhudumu wa nyumba ya kulala wageni ya Lake Hill Singida Motel  kuhusiana
 na tukio la ujambazi lililotokea kwenye hoteli hiyo.
  Kamanda Kamwela alisema wizi huo ulitokea juzi, saa  9:30 usiku, 
ambapo watu ambao idadi bado haijajulikana wakiwa na bunduki  walivamia 
hoteli hiyo na kuwapora wapangaji vitu mbalimbali.
  Alisema watu hao walipofika katika hoteli hiyo  walifyatua risasi 
hewani kwa lengo la kuwatisha wapangaji na walinzi na  kufanikiwa 
kuwafunga kamba walinzi wote watatu na kuingia katika vyumba viwili  na 
kuwanyang’anya wapangaji mali pamoja na fedha.
  Aliwataja wanaoshikiliwa kwa tuhuma hizo ni walinzi hao  wa kampuni 
binafsi ya ulinzi ya Mass Security ya mjini Singida ambao ni Juma  
Mwangwi (35), Zakaria Pastory (23) na Donald Samson (19) na Mhudumu wa 
hoteli  hiyo, Alistides Salvatory  (24).
  Kamanda Kamwela alitaja vitu vilivyoporwa kuwa ni  kompyuta mpakato 
moja, simu tatu za mkononi zenye thamani ya sh milioni moja,  saa mbili 
za mkononi moja yenye thamani ya dola 500 za Marekani  pamoja na fedha 
taslimu sh 800,000 na dola  500
Chanzo;Tanzania Daima Ofisi ya mtendaji Kondoa yafungwa
OFISI ya mtendaji wa kijiji cha Salanka, kata ya Salanka, wilayani 
Kondoa, imefungwa kwa kukosa mtendaji wa kijiji kwa muda wa mwaka moja 
sasa.
  Hali hiyo imeelezwa kuchangia wananchi kukosa huduma hivyo na 
kulazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma hiyo kwenye ofisi ya 
kata.
  Mtendaji wa kijiji hicho alisimamishwa na mkutano wa kijiji kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za kijiji.
  Akizungumza kwenye mkutano wa kijiji, Mwenyekiti wa kijiji hicho, 
Khamis Majaliwa, alisema wamekuwa wakifuatilia suala hilo kwa muda sasa 
huku Ofisi ya Mkaguzi wa Hesabu za Ndani wa halmashauri hiyo akifika 
mara moja na hadi sasa hajafika kijijini hapo kwa madai ya kukosa 
usafiri.
  Katika mkutano huo, wanakijiji hao waliazimia kwenda kuonana na Waziri
 Mkuu kutatua tatizo hilo lililodumu kwa muda wa mwaka sasa licha ya 
viongozi mbalimbali kuulizwa na kukosa majibu.
  Alipoulizwa Mkuu wa Wilaya hiyo, Omar Kwang’, alisema kwa wakati huo 
alikuwa yuko nje ya ofisi akiwa likizo na kumtaka mwandishi kusuburi 
hadi atakaporudi ofisini ndipo atatoa majibu.
Chanzo;Tanzania Daima MSIMAMO WA CHADEMA MKOA WA SINGIDA DHIDI YA MAAMUZI YA KAMATI KUU - TAARIFA KWA UMMA
WILFRED NOEL KITUNDU
MWENYEKITI CHADEMA MKOA SINGIDA
S.L.P 260
3.12.2013
KATIBU WA CHADEMA MKOA
S.L.P 260
SINGIDA
YAH: - KUJIUZURU UENYEKITI MKOA SINGIDA
Somo hapo lahusika,
Ninapenda kukuarifu kuwa nimeamua kujiuuzuru nafasi yangu ya uenyekiti wa mkoa ambayo nimekuwa nikiitumikia kwa kipindi kirefu sasa kama kielelezo cha kuamini na kudai demokrasia ya kweli ndani ya chama.
Ikumbukwe kwamba mimi ndio mwanachama wa kwanza kujiunga na CHADEMA mkoa wa SINGIDA na ni mwanachama wa 300 kitaifa, hiyo ni heshima kubwa sana kwangu na sipo tayari kuipoteza kwa kukubali kuwa sehemu ya udharirishaji huu wa demokrasia uliopitiliza
Maamuzi na vitendo vinavyoendelea ndani ya chama chetu kwa sasa ni ubakaji na udharirishaji wa demokrasia ya kweli tunayoihubiri mbele ya umma.
Kwa barua hii basi, nimeonelea bora upate ufahamu huo kuwa si vema mimi kuendelea kupingana na dhamira yangu inayonituma kuwa mwanademokrasia wa kweli.
Kwa kipindi hiki kifupi mnaweza mkaendelea kuitumia anuani yangu ya posta mpaka hapo mtakapopata anuani yenu tayari.
Ninatanguliza shukrani zangu za dhati kwa wanachadema wote wanaopinga upuuzi huu uliofanywa na kamati kuu ya chama.
Kusimamia haki, katiba na misingi ya chama ni wajibu wangu, hivyo kwa namna yoyote ile sitaweza kuwa tayari kufumba macho pindi ujinga wa namna hii unapoendelea kutekelezwa kwa uwoga wa uchaguzi.
Nakutakia kila la heri kwenye majukumu yako.
………………………………………………….
Wilfred N. Kitundu
MKOA SINGIDA
S.L.P 260
3.12.2013
Wajasiriamali waelezwa umuhimu wa soko la hisa
Kwa mujibu wa mkuu huyo, dhima ya kupata rasilimali na kuzitumia 
kikamilifu kwenye miradi yenye tija, husababisha ukuaji wa uchumi na 
kuongeza utajiri.
Dk. Kone amebainisha hayo juzi mjini Singida wakati akifungua semina 
ya siku mbili kwa wafanyabiashara na wajasiriamali juu ya soko la kukuza
 ujasiriamali (EGM) iliyofanyika kwenye ukumbi wa Aque Vitae.
Alisema ni muhimu ieleweke wazi kwamba kuna uhusiano wa moja kwa moja
 baina ya mafanikio ya masoko ya mitaji na uchumi wa nchi na kusisitiza 
kwamba moja ya sababu ni serikali kuanzisha na kusaidia maendeleo ya 
Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).
Aidha, alibanisha kwamba kampeni hiyo imekuja wakati muafaka ambao 
serikali imepania kujenga sekta binafsi imara itakayokuwa injini ya 
uchumi wa taifa.
“Napenda kuchukua fursa hii kuwahakikishia kwamba serikali inatambua 
mchango wa wadau mbalimbali katika maendeleo ya masoko ya hisa hapa 
nchini, mwamko kama huu unalenga kujenga uelewa kwa sekta binafsi na 
umma juu ya fursa zipatikanazo na soko la hisa zinaungwa mkono na 
serikali.
“Pia nitumie fursa hii kuwataka wadau na wahusika wote kwa ukamilifu 
wenu kutumia tukio hili ili kutumia fursa zipatikanazo kwenye soko la 
hisa,” alisema Dk. Kone.
Hata hivyo Dk. Kone alisema tafiti nyingi zimeonyesha kwamba 
upatikanaji wa mitaji ya wajasiriamali wadogo na wa kati ni changamoto 
kwa maendeleo ya kukua kwa shughuli za ujasiriamali na sekta hiyo kwa 
ujumla.
Awali Meneja Uhusiano wa kitaasisi kutoka DSE, Mary Mniwasa, 
alimweleza mkuu wa mkoa kuwa lengo la semina hiyo ni kampeni ya umma ya 
kupunguza umaskini hapa nchini.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Singida, Francis 
Mashuda, alisema wafanyabiashara wanakumbana na changamoto kubwa ya 
ukosefu wa mitaji.
Semina hiyo ilitarajiwa kuhudhuriwa na wafanyabiashara wa kada 
mbalimbali na wajasiriamali wasiopungua 65, imefadhiliwa na DSE chini ya
 uratibu wa TCCIA Mkoa wa Singida.
Chanzo;Tanzania Daimma Singida watakiwa kuchangamkia Soko la Hisa
 WAJASIRIAMALI
 na wafanyabiashara mkoani Singida wametakiwa kuchangamkia fursa 
zilizopo Soko la Hisa la Dar es Salaam ili kuboresha na kuendeleza 
biashara zao.
Mwito
 huo ulitolewa juzi na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone wakati 
akifungua semina ya siku mbili juu ya Soko la kukuza ujasiriamali 
iliyofanyika ukumbi wa Aqua Vitae mjini hapa.
Dk
 Kone alisema kuwa Soko la Hisa la Dar es Salaam kupitia kitengo chake 
kipya kijulikanacho kama “Soko la Kukuza Ujasiriamali”, ni suluhisho la 
upatikanaji wa mitaji kwa wajasiriamali kote nchini.
Alisema
 kuwa soko hilo litatoa suluhisho kwa changamoto zinazowakabili 
wajasiriamali katika upatikanaji wa uhakika wa mitaji ya muda mrefu kwa 
ajili ya kuendeleza biashara zao, jambo ambalo limekuwa likiwasumbua 
wajasiriamali na wafanyabiashara.
“Kwa
 hiyo basi, soko la kukuza ujasiriamali litasaidia kuleta msukumo wa 
utekelezaji sera mbalimbali za serikali zinazolenga kuondoa changamoto 
hizo na kuleta urahisi wa upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya kukuza 
biashara zao,” Dk Kone alisema.
Aidha,
 alieleza kuwa soko hilo linatarajiwa kulichangamsha soko kwa ujumla 
kupitia ongezeko la utoaji na uorodheshaji wa hisa, kupanua wigo na 
fursa za kuwekeza mitaji na kuongeza ari ya wananchi kujiwekea akiba.
Kwa
 mujibu wa mkuu wa mkoa huo, baadhi ya faida ziletwazo na soko hilo ni 
kupunguziwa kodi katika gawio, kusamehewa kodi kwenye ongezeko la 
thamani ya mtaji na ushuru wa stempu na punguzo kodi ya makampuni.
Chanzo;Habari Leo 
Wavamia nyumba, wazichoma moto
MWENYEKITI wa Kijiji  cha Makunda, Kata ya Kyengege, wilayani Iramba
 kwa kushirikiana na watu wengine  zaidi ya 50 wamevamia na kuchoma moto
 nyumba mbili za wakulima wakipinga kuwa  si wazaliwa wa eneo hilo na 
kujipatia ardhi zaidi ya ekari 285.
  Habari za uhakika kutoka katika eneo la tukio  hilo zinaeleza tukio 
hilo limetokea juzi, saa 8:00 mchana katika mashamba ya  kilimo Kijiji 
cha Makunda.
  Kwa mujibu wa habari  hizo, siku ya tukio watuhumiwa wakiwa na silaha 
za jadi walivamia makazi ya  mkulima mwezao, Esau Talanzia (47) na 
kuchoma moto nyumba yake.
  Pia walichoma magunia  sita ya mahindi, magunia mawili ya alizeti 
godoro moja, fedha taslimu sh  450,000 na vitu vingine vilivyokuwemo, 
vyote vikiwa na thamani ya sh milioni  1.8.
  Pia katika tukio hilo  nyumba moja ya Matayo Kizaberga, mkulima na 
mkazi wa Makunda-Mbugani ilichomwa  moto na vitu vyote vilivyokuwemo 
kuteketea.
  Kamanda wa Polisi wa  Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela, alithibitisha 
kutokea kwa tukio hilo na kwamba  watu 25 akiwamo mwenyekiti wa kijiji 
wanashikiliwa na polisi kuhusiana na tukio  hilo.
  Kamanda Kamwela alisema  chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa mashamba 
ambapo wanakijiji cha Makunda  wanapinga waathirika hao kumiliki ekari 
284 wakati si wazawa wa eneo hilo.
  Alisema watuhumiwa wanatarajiwa kufikishwa  mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.
Chanzo;Tanzania Daima 
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu watakiwa kufika kijiji cha Kazamoyo
Baadhi
 ya wananchi wakiwa wamehamishia makazi yao chini ya mti uliopo kwenye 
korongo kijiji cha Handa mpakani mwa Wilaya ya Chemba na Singida 
Vijijini mara baada ya nyumba zao kuchomwa moto na askari polisi na wale
 wa kikosi cha kupambana na ujangili kwa madai ya kuvamia hifadhi ya 
msitu wa mgori (PICHA NA HILLARY SHOO).
 Huyu
 ni mmoja wa watoto walionashwa na kamera yetu akiwa amelala hoi kwa 
kukosa chakula na huduma zingine, baada ya nyumba zao kuchomwa moto 
wakati wa operesheni ya kuwahamisha katika kitongoji cha Kazamoyo kwa 
madai ya kuvamia hifadhi, hata hivyo wananchi hao wameisha katika eneo 
hilo kwa zaidi ya miaka nane toka mwaka 2005 , lakini sheria ya kuingiza
 eneo hilo kwenye msitu wa hifadhi ya mgori ilifanyika mwaka 2007, 
(PICHA NA HILLARY SHOO).
.Unyanyasaji dhidi ya wananchi wakithiri wilayani Singida 
Na Hillary Shoo, Singida
KITUO
 cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wametakiwa kufika katika 
kitongoji cha Kazamoyo kijiji cha Nguamuhanga tarafa ya Mgori Wilayani 
Singida vijijini na kujionea unyanyasaji dhidi ya wananchi wakati wa 
zoezi la kuwaondoa katika hifadhi ya msitu wa mgori.
Hayo
 yamesemwa juzi katika kitongoji hicho na baadhi ya wananchi walioamua 
kuhamia kwenye korongo na kuishi chini ya miti kama digidigi kunusuru 
maisha yao kutokana na vipigo kutoka kwa wa kikosi cha kupambana na 
ujangili Wilaya ya Singida na askari polisi.
Wamesema
 ni vyema kituo hicho wakafika mapema ili kuona jinsi ambavyo binadamu 
wanavyoishi maisha ya shida ta taabu kwenye eneo hilo kufuatia amri ya 
mkuu wa Wilaya ya kuhamisha kwa muda mfupi.
Wamesema
 eneo hilo wameishi zaidi ya miaka nane na kujenga makazi bora bila 
matatizo yoyote, lakini jambo la ajabu ni baada ya Wilaya ya Chemba na 
Sngida kuwekeana mipaka na kuonekana kuwa wako Singida.
“Wakati
 tuko kijiji cha Handa Wilaya ya Chemba, tuliishi bila matatizo lakini 
baada ya kuhamia singida ndipo mambo yalianza kubadilika na kuambiwa 
kuwa tuko eneo la hifadhi, hii ni ajabu sana , Wilaya moja tuliishi 
vizuri hii nyingine haitutaki sasa tuende wapi.” Alihoji mmoja wa kina 
mama.
Licha
 ya kukosa huduma muhimu kama vile maji, mahema, vyoo baadhi ya kina 
mama na watoto walionekana wakiwa katika huzuni klubwa huku wengine 
wakiangua vilio baada ya kuwaona waandishi wa habari wakidhani kuwa ni 
askari.
Hata
 hivyo eneo hilo lina mbu wengi, jua kali na mbaya zaidi hivi sasa ni 
msimu wa mvua katika maeneo hayo, je swali la kujiuliza wataishije hapo 
wananchi hao zaidi ya 1,000 ambao nyumba zao zimechomwa moto.
Hata
 hivyo Mkuu wa Wilaya ya Singida Qeen Mlozi amesema zoezi hilo 
linaendelea sanjari na kuhakikisha wanaondoka kwenye korongo hilo 
walimojificha.
Hivi
 karibuni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu 
alitembelea eneo hilo la kusitisha zoezi la kuwahamisha mpaka pale 
kamati ya kudumu ya huduma za kijamii ya baraza la madiwani 
watakapokutana kutoa maamuzi sahihi juu ya wananchi hao.
Hata
 hivyo agizo hilo la Naibu Waziri limepingwa vikali sana na mkuu wa 
Wilaya ya Singida Mwalimu Qeen Mlozi kwamba Nyalandu hana mamlaka 
kisheria ya kusitisha zoezi hilo, na kwamba anayeweza kumwamuru 
kusitisha zoezi ni Mkuu wa Mkoa pekee na si vinginevyo.
Na Mo Blog 
SINGIDA SASA YAJA NA MKAKATI WA KUIBUKA KIRIADHA
Picha zote kutoka maktaba ya Singida Yetu Blog
SINGIDA ni moja kati ya mikoa ambayo ilikuwa inafanya vizuri katika mchezo wa riadha miaka ya 1980 na kutoa wanariadha mahiri ambao waliiwakilisha Tanzania katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.
Mkoa huo ni wenye mandhari nzuri yenye mawe mawe pamoja na mto upande wa kushoto na kulia hususan pale unapofika mkoani hapo.
Hakika mkoa huu ni wenye vitu vingi, lakini kikubwa zaidi ni wakimbiaji wa riadha hususan maeneo ya Singida Vijijini ambako kama wakimbiaji hao wataweza kupewa vifaa maalumu kwa ajili ya kukimbia na wadau wa riadha wakajitokeza na kuchangia zaidi katika riadha, Tanzania itakuwa na medali nyingi na kupata heshima katika nchi mbalimbali duniani.
Nasema hivyo kwa sababu hivi karibuni Mbunge wa Singida Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu aliandaa mashindano ya riadha hususan vijijini kwa ajili ya kuibua vipaji kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Shrika la African Wildlife Trust (AWT), Pratic Patel.
Mbio hizo zilizojulikana kwa jina la Singida Marathon za kilometa 21, zilianza rasmi Novemba 9, mwaka huu kwa kushirikisha wakimbiaji zaidi ya 400 kutoka Singida Mjini na Singida Vijijini na zilianzia Kijiji cha Mitula, Kata ya Kinyagigi na kuishia Viwanja vya Shule ya Msingu Ntunduu (W) Singida Vijijini.
Mbio hizo zilikuwa za kilometa 21 ambazo ni nusu marathoni na kilometa 5 na mwisho kabisa ni kilometa 2.5 ambazo ziliwashirikisha watoto wa kiume na wa kike. Wakimbiaji walikuwa wamejiandaa wenyewe na walijiandikisha, lakini baadhi yao pamoja na kukabiliwa na ukosefu wa viatu, lakini waliweza kumudu hali hiyo kutokana na mazingira waliyokua nayo na kuonesha vipaji vyao vilivyowashangaza wengi.
Inawezekana kukimbia bila viatu ni jambo lisiloruhusiwa, lakini kutokana na mazingira yenyewe ya vijijini hali hiyo haikuwa kikwazo kwa wakimbiaji hao kukimbia bila viatu ila walionesha kuwa wana moyo na nia ya dhati kuonesha vipaji vyao hakika ilikuwa faraja kubwa kwao kwani mwisho wa siku waliweza kuibuka washindi na wengine wakapata kifuta jasho.
Washindi hao ni Paulo Itambi ambaye aliibuka mshindi wa kwanza kwa upande wa wanaume ambaye alipewa zawadi ya Sh 300,000, Emmanuel Samson wa pili (Sh 200,000) na Samwel Ikungi wa tatu (Sh 100,000). Kwa upande wa wanawake, mshindi wa kwanza Fabiola William (Sh 300,000), Zakia Abdallah (Sh 200,000) na Winfrida Hassani (Sh 100,000).
Mbio za kilometa tano, washindi ni Gabriel Garado (Sh 200,000), Deo Lazaro (Sh 100,000) na Jonas John (Sh 50,000) huku wanawake ni Neema Kisuda (Sh 200,000), Pascalina Silvesta (Sh 100,000) na Christina Yuda (Sh 50,000) ambao washindi wa kilometa 2.5 wakiwa ni Julita Antony (Sh 100,000), Editha Gabriel (Sh 50,000) na Magreth Bernado (Sh 25,000).
Wanaume walikuwa ni Petro Pascal mshindi wa kwanza na kupewa Sh 100,000, Baraka Sebastian (Sh 50,000), Haji Swalehe (Sh 25,000) huku washindi wengine 400 kila mmoja akipewa Sh 10,000. Baada ya washindi hao kukabidhiwa zawadi zao, Patel ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Naibu Waziri Nyalandu, alikabidhi pia medali mbalimbali kwa washindi hao.
Aidha, alitoa changamoto kwa
wananchi hao kuacha tabia ya kuua tembo, bali wanastahili kulindwa na kuhifadhiwa ili kukuza uchumi na kufungua milango ya ajira.
Hata hivyo, baadhi ya washindi walimshukuru Nyalandu kwa kuamua kuanzisha mashindano hayo maeneo ya vijijini ili kuibua vipaji na kutoa rai kwa wadau wa riadha mkoani humo pamoja na sehemu mbalimbali kuanzisha klabu za michezo ya riadha ili kuendeleza vipaji na kuibuavipaji vipya.
Fabiola ambaye ni mkimbiaji mashuhuri wa riadha na aliyeiletea sifa Tanzania, alisema awali alikuwa akikimbia mkoani Kilimanjaro, lakini hivi sasa yupo Singida ambako alihamia Singida Vijijini kwenye Jimbo la Nyalandu, ndio kwao alipozaliwa na anaona fahari kubwa kuona wilaya hiyo ina wakimbiaji wengi na ni wazuri, lakini bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa vifaa kwa ajili ya kufanyia mazoezi.
Fabiola na wadau wengine wamemwomba Naibu Waziri pamoja na wadau wengine kushirikiana kwa pamoja ili kuanzisha klabu za michezo ya riadha ili kuibua vipaji vya wakimbiaji waliopo maeneo ya vijijini.
Alisema mkoa huo una wanamichezo wengi, lakini hakuna klabu za michezo hali inayosababisha baadhi ya wanariadha kufanya mazoezi bila ya kuwa na vifaa maalumu, lakini walimpongeza Nyalandu kwa kuanzisha mashindano hayo maeneo ya vijijini ili kuibua wanamichezo wengi watakaoweza kuutangaza mkoa huo pamoja na Tanzania kwa ujumla pale yanapotokea mashindano ya riadha ya ndani na nje ya nchi.
Kung’olewa kwa Zitto, Mkumbo: Chadema mikoani watofautiana
Wanachama wa Chadema mikoa mbalimbali nchini pamoja na wananchi 
wametoa maoni tofauti kuhusu uamuzi wa Kamati Kuu ya chama hicho wa juzi
 kuwavua uongozi viongozi wake watatu; Naibu Katibu Mkuu wake Zitto 
Kabwe na Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk Kitila Mkumbo na mwenyekiti wa chama 
hicho Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.
Singida
Kutoka mkoani Singida, uongozi wa chama hicho  
jana ulifanya kikao cha faragha kujadili uamuzi wa chama hicho, huku 
baadhi ya wananchi wakiuelezea uamuzi  huo kuwa umetokana na pupa na 
kushindwa kuvumiliana, wengine wakitishia kujitoa katika chama hicho.
Kwa zaidi za saa 5 uongozi huo ulikuwa ukijadili 
hatua hiyo huku ukiahidi kutoa taarifa yake baada ya kikao hicho 
kilichokuwa kikiendelea hadi baada ya saa 7 mchana.
Habari zaidi kutoka Wilaya ya Iramba mkoani humo 
zinasema kuwa wanachama wa Chadema wilayani humo wametishia kurudisha 
kadi za chama hicho kilichokuwa kimeanza kujizolea umaarufu wakisema 
watafanya hivyo ikiwa Chadema ‘watalitosa jembe’ lao.
Baadhi ya wananchi waliozungumza na gazeti hili 
walisema kuwa hatua hiyo inaweza kuipunguzia umaarufu Chadema na kwamba 
ustawi wa vyama vingi vya siasa unaponzwa na pupa, jazba hata kukosa 
uvumilivu.
“Kikundi hiki cha viongozi kinasababisha Chadema 
kumeguka kama tulivyosikia juzi. Kwa maoni yangu kabla hakijawavua 
uongozi Zitto, Dk Mkumbo na Mwigamba, kilikuwa kinashabikiwa na asilimia
 90, hapa Singida, lakini baada ya tukio la juzi la kuwavua uongozi 
baadhi ya viongozi, nina hakika kinashabikiwa na asilimia 30 ya 
wananchi,” alisema Juma Mdida.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TLP Wilaya ya 
Singida, Athumani Nkii, alisema kuwa ustawi  wa vyama vingi vya siasa 
unaponzwa na vitendo vya pupa, jazba na ubinafsi wa baadhi ya viongozi 
wake baada ya majina yao kupata umaarufu,wakisahau kuwa umaarufu huo 
unachangiwa na chama husika.
“Kwa upande wa Kabwe Zitto, nadhani safari zake za
 nje ya nchi na suala la mapesa ya Uswisi, zitakuwa hazina baraka za 
Chadema. Kuhusu Dk Kitila Mkumbo, sina kabisa fununu ya madhambi 
yake,”alisema.
Rukwa 
Barua ya kujiuzulu nafasi ya Makamu Mwenyekiti 
Chadema Tanzania Bara, Said Amour Arfi ambaye pia ni Mbunge wa Mpanda 
imesambazwa  kwa wapiga kura wake na wananchi wa jimbo hilo ili  
wafahamu sababu za msingi za yeye kujiondoa katika nafasi yake.
                
              Katibu wa mbunge huyo, Joseph Mona, alipata taarifa za uamuzi huo wa ghafla, aliosema kuwa ni sahihi.
Chanzo;Mwananchi 
KATA YA MTAMAA MANISPAA YA SINGIDA YAPATA NEEMA YA UMEME.
Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa CCM Bw. Hassan Mazala 
(Picha Kutoka Maktaba Yetu)
Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa CCM Bw. Hassan Mazala wakati akizungumza na wananchama wa CCM katika kata hiyo ambapo amesema upembuzi yakinifu juu ya mradi huo unatarajiwa kuanza mwezi huu.
Amesema kuwa endapo umeme ukiunganishwa katika kata hiyo kutasaidia wananchi kujishughulisha na shughuli za kiuchumi ambazo zinategemea nishati hiyo na hatimaye kuondokana na umasikini wa kipato unaowakabili wakazi wa kata hiyo
Aidha Bw Mazala ametoa wito kwa wananchi wa kata hiyo kuwa tayari kuonyesha nia ya kuhitaji huduma hiyo kwa kujiandikisha hali ambayo itaongeza juhudi za mradi huo wa REA kwenda kasi kutokana na mahitaji ya idadi kubwa ya watu.
Na Singida yetu Blog 
SEMA yagharamia ujenzi wa Vyoo katika shule tano za Manispaa ya Singida.
Meneja
 wa shrika la SEMA, Ivo Manyanku,(wa kwanza kulia) akitoa taarifa yake 
ya ujenzi wa vyoo bora katika shule tano za msingi manispaa ya Singida 
kwa Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu), Mh. Kassim Majaliwa (mwenye 
miwani).Vyoo hivyo vimegharimu zaidi ya shilingi 155 milioni.
Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu) Mh. Kassim Majaliwa (aliyeipa kisongo kamera) akizindua rasmi ujenzi wa vyoo bora katika shule ya msingi Unyankindi.Vyoo hivyo bora vimejengwa kwa gharama ya shilingi 155 milioni na shirika la SEMA.Kushoto ni meneja wa SEMA. Ivo Manyanku.
Naibu Waziri wa TAMISEMI (Elimu),Kassim Majaliwa akikata utepe kuashiria ufunguzi wa matumizi ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi mjini Singida.Vyoo hivyo vimejengwa na shirika la SEMA kwa gharama ya shilingi 155 milioni.
Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu) Mh. Kassim Majaliwa (aliyeipa kisongo kamera) akizindua rasmi ujenzi wa vyoo bora katika shule ya msingi Unyankindi.Vyoo hivyo bora vimejengwa kwa gharama ya shilingi 155 milioni na shirika la SEMA.Kushoto ni meneja wa SEMA. Ivo Manyanku.
Naibu Waziri wa TAMISEMI (Elimu),Kassim Majaliwa akikata utepe kuashiria ufunguzi wa matumizi ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi mjini Singida.Vyoo hivyo vimejengwa na shirika la SEMA kwa gharama ya shilingi 155 milioni.
Moja ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi manispaa ya Singida vilivyojengwa na shirika la SEMA la mkoa wa Singida.
Shirika
 lisilo la kiserikali la Sustainable Environment Management Action 
(SEMA) la mkoani Singida limetumia zaidi ya shilingi 155 milioni 
kugharamia ujenzi wa vyoo bora katika shule tano za manispaa ya Singida.
 Shule zilizonufaika na mradi huo ni,Unyankindi,Singidani,Manguamitogho,Mtamaa na Mtisi.
 Hayo 
yamesemwa juzi na Meneja wa SEMA, Ivo Manyanku wakati akizungumza kwenye
 hafla iliyofana ya uzinduzi wa vyoo hivyo uliofanyika katika shule ya 
msingi Unyankindi Singida mjini.
 Amesema
 fedha hizo zilizotumika katika ujenzi huo zimetolewa ufadhili na 
shirika la WaterAid Tanzania kwa ajili ya kutekeleza mradi wa maji na 
usafi shuleni katika halmashauri ya manispaa ya Singida.
 “Vyoo
 hivi vina matundu 48 ambayo yana uwezo wa kuhudumia wanafunzi 2,903 
kati yao wavulana ni 1,446 na wasichana ni 1,457.Idadi hiyo inajumuisha 
na walemavu 38 ambao 25 ni wavulana na 13 ni wasichana”,amesema Meneja 
huyo.
 Kwa 
upande wake mgeni rasmi katika uzinduzi huo,naibu waziri TAMISEMI 
(elimu),Kassimu Majaliwa,alitumia fursa hiyo kulipongeza shirika la SEMA
 kwa ujezi bora wa vyoo hivyo ambavyo vimekidhi vigezo vyote 
vinavyohitajika.
 Amesema
 serikali na wadau wengine wa maendeleo hawana budi kuliunga mkono 
shirika la SEMA kwa madai linatelekeza miradi yake kulingana na thamani 
ya fedha zilizotumika.
 “SEMA binafsi nawapongezeni sana ujenzi huu mtakuwa mmeisaidia serikali katika kupunguza 
kero
 mbalimbali zinazoikabili sekta mbalimbali ikiwemo ya elimu.Vyoo hivi ni
 bora mno na vitakuwa vimepunguza kwa kiwango kikubwa uhaba wa vyoo 
katika shule zetu za msingi”,amesema Majaliwa.
 Wakati
 huo huo, Naibu Waziri huyo ameuomba uongozi wa halmashauri ya manispaa 
ya Singida kusimamia matumizi ya vyoo hivyo ili viweze kutumika kwa muda
 mrefu zaidi.
Chanzo: Singida yetu  









