Home » » AFUNGWA MIAKA 60 JELA KWA KOSA LA UNYANG’ANYI NA KUBAKA

AFUNGWA MIAKA 60 JELA KWA KOSA LA UNYANG’ANYI NA KUBAKA

Mwandishi wetu, Singida Yetu
MAHAKAMA ya hakimu mkazi mjini Singida imemhukumu mwanaume mmoja   kifungo cha miaka 60 jela baada ya kumtiwa hatiani kwa makosa ya unyang’anyi na kubaka.
Aliyekumbwa na adhabu hiyo ametajwa kuwa Omari Msawila (50) mkazi wa eneo la Minga  katika Manispaa ya Singida.

Mapema mwendesha mashitaka Geofry Luhanga alidai kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo siku ya disemba 30 mwaka jana majira ya saa 6.15 usiku huko maeneo ya Karakana Singida mjini
Mbele ya hakimu Chiganga Tengwa   wa mahakama hiyo ilidaiwa kuwa mshitakiwa akiwa na wenzake ambao hadi sasa hawajakamatwa walivunja nyumba ya mtu mmoja kisha kuingia ndani.
Ililelezwa kuwa   mshitakiwa na wenzake walinyang’anya shilingi 90,000 taslimu pamoja na mali mbalimbali ikiwemo madebe matatu ya mahindi kisha kumbaka mke wa mlalamikaji kabla ya kutoweka.
 Akitoa hukumu hiyo, hakimu Tengwa amesema kutokana na kuridhishwa  bila kuacha shaka lolote na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka, mshitakiwa atatumikia  kifungo cha miaka 30 jela kwa unyang’anyi na miaka mingine kama hiyo kwa kosa la kubaka.
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa