Home » » MBALI NA KASORO NDOGO MTIHANI WA DARASA LA SABA SINGIDA WAANZA VYEMA.

MBALI NA KASORO NDOGO MTIHANI WA DARASA LA SABA SINGIDA WAANZA VYEMA.



Na.Nathaniel Limu-Singida.
Mtihani  wa kumaliza elimu ya msingi unaohusisha wanafunzi 27,749 wa darasa la  saba mkoani Singida umeanza kwa amani na utulivu licha ya  kujitokeza kwa kasoro ndogondogo.
Miongoni mwa kasoro hizo ni pamoja na  utoro, baadhi ya wanafunzi kutojua  kusoma na kuandika na walimu na wasimamizi kulalamikia mfumo wa maswali ya kuchagua na kuweka vivuli.
Katika  shule ya msingi  Mtisi  iliyopo umbali wa zaidi ya kilomita 24 kusini magharibi mwa mji wa Singida, wasimamizi  wa mtihani huo wamesema kati ya 34 watahiniwa nane (8) hawakufanya mtihani kutokana na utoro na wengine sita wameshindwa kusoma wala kuandika.
Hata  hivyo afisa elimu mkoa wa Singida  Yusuf  Kipengele, amesema mbali ya kasoro hizo  hakuna dosari nyingine kubwa iliyojitokeza na kuathiri ufanyaji huo wa mtihani ulioanza leo.
Kipengele ametoa wito kwa wasimamizi  wa mtihani  huo kuwa waadilifu na kutojihusisha na udanganyifu vinginevyo watachukuliwa hatua za kisheria pindi watakapobainika. 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa