Home » » SACCOS 7 MKOANI SINGIDA ZAFANIKIWA KUPATA MIKOPO YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 1.4 KUTOKA CRDB.

SACCOS 7 MKOANI SINGIDA ZAFANIKIWA KUPATA MIKOPO YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 1.4 KUTOKA CRDB.


Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi vyeti kwa viongozi wa SACCOS saba za mikoa ya Singida na Manyara. Vyeti hivyo vimetolewa na mfuko wa uwezeshaji (Wananchi Empowement Fund) baada ya SACCOS hizo kufanikiwa mikopo ya thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.4.
Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt.Parseko Kone akikabidhi cheti kwa viongozi wa SACCOS ya Jipe Moyo ya kata ya Kinyangiri wilayani Mkalama.
Katibu Mtendaji wa baraza la taifa la uwezeshaji wananchi kiuchumi Dk. Anacleti Kashuliza akitoa taarifa yake kwenye hafla ya kukabidhi vyeti kwa SACCOS saba za mkoa wa Singida na Manyara. Wa kwanza kushoto ni mkuu wa mkoa wa Singida na wa kwanza kulia ni mkuu wa wilaya ya Singida Queen Mlozi. 
Meneja mikopo wa CRDB tawi la mkoa wa Singida Mbwana Hemed akitoa salamu zake kwenye hafla ya kukabidhi vyeti kwa SACCOAS saba za mkoa wa Singida na Manyara.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria hafla ya kukabidhi vyeti kwa SACCOS za mkoa wa Singida na Manayara. Wa kwanza kushoto ni Halima Jamal wa gazeti la Tanzania Daima akifuatiwa na Abbya Nkungu wa Habari Leo na Daily News pia ni Katibu wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Singida. Wa kwanza kulia ni Elisante John wa Radio Cluods na Nipashe na wa pili kulia ni Awilla Sila wa Mwananchi na The Citizen.
Baadhi ya viongozi wa SACCOS za mkoa wa Manyara na Singida, wakipata ‘msosi’ muda mfupi baada ya kukabidhiwa vyeti na mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone.(Picha na Nathaniel Limu).
Na. Nathaniel Limu
Benki ya CRDB tawi la mkoa wa Singida imetoa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi biloni 1.4 kwa SACCOS saba za mkoa wa Singida na Manyara.
Akizungumza kwenye hafla ya utoaji wa vyeti kwa SACCOS za mikoa ya Manyara na Singida zilizopta mikopo kutoka mfuko wa uwezeshaji (Mwananchi Empowerment Fund), Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone amesema SACCOS nne za mkoa wa Singida, zimekopeshwa zaidi ya shilingi milioni 255.5 sawa na aslimia 3.32 ya fedha hizo, wakati SACCOS tatu za mkoa wa Manyara zenyewe zimekopeshwa zaidi ya shilingi bilioni 1.2.
Kuhusu marejesho, Dkt. Kone amesema hadi kufikia Julai 31 mwaka huu, kiwango cha urejeshaji kilifikia aslimia 94.4.Kwa upande wa mkoa wa Singida pekee, kilifikia asilimia 91.7.
 Amesema hata hivyo ipo tatizo la urejeshaji kwa SACCOS ya Kumekucha ya Itigi Manyoni ambayo ilikopeshwa jumla ya shilingi 84,472,000.
Fedha hizo  zilipaswa ziwe zimerejeshwa kabla ya Agosti 31 mwaka huu, lakini hadi  sasa SACCOS hii inadaiwa shilingi 21,168,000 ambazo ni asilimia 25 ya mikopo iliyotolewa kwa mkoa wa Singida.
Dkt .Kone amesema mbaya zaidi ni kwamba wengi wa viongozi  wa SACCOS hiyo ni miongoni mwa wadaiwa sugu wa mikopo hiyo.
SACCOS za Lusilille  na Tumaini za Manyoni na Jipe moyo ya Iramba zilishamaliza kurejesha mikopo yao.
Kwa upande wao viongozi wa SACCOS hizo wameomba muda wa kurejesha mikopo uongezwe zaidi ili waweze kupata muda wa kutosha kupata faida ya itakayotosheleza  kulipa mikopo na kubakiwa na akiba ya kukidhi mahitaji.
MO BLOG

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa