Home » » USALAMA BARABARANI SINGIDA WAKUSANYA MILIONI 53

USALAMA BARABARANI SINGIDA WAKUSANYA MILIONI 53

Mwandishi wetu, Singida Yetu

KIKOSI  cha askari wa usalama  barabarani  mkoani Singida kimekusanya  zaidi ya shilingi  milioni 53.1  kutokana na  faini mbalimbali  zilizotozwa kwa wadau  wa usafiri  na usafirishaji  kwa kipindi cha mwezi mmoja  uliopita.

Kamanda  jeshi la polisi mkoani humo Kamishina msaidizi  Linus Sinzumwa amesema fedha hizo  zimetokana na  makosa 1842 ya kukiukwa kwa sheria, taratibu na kanuni  za usalama  barabarani.

Kamanda Sinzumwa ameyataja baadhi ya makosa hayo kuwa ni pamoja na mwendo kasi kwa madereva,  kutofunga mkanda, ulevi wakati wa kuendesha gari, kutokuwa na  kibali cha barabarani, magari mabovu na  kutozingatia alama za usalama barabarani.

Ametoa wito kwa wadau wote   sekta ya  usafiri na usafirishaji  kujenga uatamaduni wa kuzingatia sheria zote muhimu ili kupunguza ajali hususani katika kipindi hiki cha kuelekea kuadhimisha  wiki  ya nenda kwa usalama barabarani.

Hivi sasa jeshi la polisi mkoani singida lipo kwenye mchakato wa ukaguzi wa vyombo vyote  vya moto ikiwa ni moja ya hatua muhimu katika kuadhimisha wiki  hiyo

Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa