Mwandishi
wetu, Singida Yetu
WAZAZI katika
halmashauri ya Manispaa ya Singida wamelalamikia mavazi yanayovaliwa na
wanafunzi wa vyuo vya uhazili na uhasibu  vilivyopo katika  mji wa
Singida kwa madai  kuwa  yanachangia kuharibu  na kuleta 
mmomonyoko wa maadili  kwa  watoto.
Wakizungumza kwenye viwanja vya shule ya Sekondari ya Utemini katika kikao chao na mkuu wa wilaya ya Singida bibi Queen Mlozi, wazazi hao wamesema mavazi ya wanachuo hao yamekuwa kero na kusababisha mmomonyoko wa maadili kwa jamii.
Wakizungumza kwenye viwanja vya shule ya Sekondari ya Utemini katika kikao chao na mkuu wa wilaya ya Singida bibi Queen Mlozi, wazazi hao wamesema mavazi ya wanachuo hao yamekuwa kero na kusababisha mmomonyoko wa maadili kwa jamii.
Wamedai kuwa 
baadhi  ya wanafunzi  wa  kike katika  vyuo  hivyo
wanavaa nguo  fupi   sana  kinyume na maadili ya
kitanzania   ambazo zinaweza  kuwa kuchochea vitendo vya ngono.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Singida bibi Mlozi amesema ingawa hata yeye ameliona tatizo lakini ni vyema ikaeleweka kuwa hizo ni athari za utatandawazi na ni vigumu kuzizuia.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Singida bibi Mlozi amesema ingawa hata yeye ameliona tatizo lakini ni vyema ikaeleweka kuwa hizo ni athari za utatandawazi na ni vigumu kuzizuia.
Hata  hivyo
 mkuu huyo  wa wilaya ya Singida ameahidi kukutana na walimu na 
wanafunzi wa vyuo hivyo ili  kuzungumzia tatizo hilo  na kujaribu
kutafuta ufumbuzi wa suala hilo.
Blogzamikoa 
0 comments:
Post a Comment