Home » » WAZAZI WAKERWA NA ‘VI-MINI’ VYA WANAVYUO SINGIDA, WASHITAKI KWA DC

WAZAZI WAKERWA NA ‘VI-MINI’ VYA WANAVYUO SINGIDA, WASHITAKI KWA DC

Mwandishi wetu, Singida Yetu
WAZAZI katika halmashauri ya Manispaa ya Singida wamelalamikia mavazi yanayovaliwa na wanafunzi wa vyuo vya uhazili na uhasibu  vilivyopo katika  mji wa Singida kwa madai  kuwa  yanachangia kuharibu  na kuleta  mmomonyoko wa maadili  kwa  watoto.

Wakizungumza kwenye viwanja vya shule ya Sekondari ya Utemini katika kikao  chao na mkuu wa  wilaya ya  Singida  bibi Queen Mlozi,  wazazi hao wamesema mavazi  ya wanachuo hao yamekuwa kero  na kusababisha  mmomonyoko wa maadili kwa jamii.

Wamedai kuwa  baadhi  ya wanafunzi  wa  kike katika  vyuo  hivyo wanavaa nguo  fupi   sana  kinyume na maadili ya kitanzania   ambazo zinaweza  kuwa kuchochea vitendo vya ngono.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Singida  bibi Mlozi  amesema ingawa hata yeye ameliona tatizo lakini ni  vyema ikaeleweka kuwa  hizo ni athari za utatandawazi na ni  vigumu kuzizuia.

Hata  hivyo  mkuu huyo  wa wilaya ya Singida ameahidi kukutana na walimu na  wanafunzi wa vyuo hivyo ili  kuzungumzia tatizo hilo  na kujaribu kutafuta ufumbuzi wa suala hilo.
Blogzamikoa 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa