Home » » SERIKALI YA SINGIDA YAZITAKA MANISPAA KUCHANGIA UJENZI WA MAABARA ZA SHULE ZA KATA.

SERIKALI YA SINGIDA YAZITAKA MANISPAA KUCHANGIA UJENZI WA MAABARA ZA SHULE ZA KATA.




Mkuu wa wilaya ya Singida Mwalimu Queen Mlozi, akizungumza na wananchi wa kata ya Utemini manispaa ya Singida akihamasisha ujenzi wa maabara katika shule za sekondari za kata na kujitambulisha.


Diwani wa kata ya Utemini CCM jimbo la Singida mjini Baltazar Kimario, akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya shule ya sekondari kata ta Utemini. Mkutano huo ulitumika kwa Mkuu wa Wilaya Mlozi kuhamasisha ujenzi wa maabara.
 
Baadhi wa wakazi wa Utemini mjini Singida waliohudhuria mkutano wa hadhara ulioitishwa kwa ajili ya mkuu wa wilaya ya Singida Queen Mlozi, kuhimiza ujenzi wa maabara.
Mkuu wa wilaya ya Singida,mwalimu Queen Mlozi (wa kwanza kushoto) akishiriki kutoa burudani na kikundi cha uhamasishaji cha nyota njema cha Utemini, kwenye mkutano wa hadhara.(Picha na Nathaniel Limu).
 Serikali  ya wilaya ya Singida imewaagiza  wakazi wa manispaa ya Singida, kuunganisha nguvu zao pamoja kuchangia ujenzi wa maabara katika shule zote za sekondari za kata.
Kasi na nguvu zilizotumika kujenga shule za sekondari za kata, zimetakiwa ziongezeke zaidi ili ifikapo oktoba 20 mwaka huu, majengo ya maabara yawe yamefikia  katika hatua nzuri ya kupauliwa.
Agizo hilo limetolewa na mkuu wa wilaya ya Singida Mwalimu Queen Mlozi, wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Utemini jimbo la Singida mjini.
Amesema suala la ujenzi wa maabara ni muhimu mno katika wakati huu wa dunia ya sayansi na teknolojia.
Mlozi amesema wazazi na walezi ni lazima watambue hilo, ili waweze kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa maabara mahali watoto wao, watajifunza kwa vitendo masuala ya sayansi. 
Mo Blog

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa