Home » » MGOMO WA WALIMU WAENDELEA SINGIDA

MGOMO WA WALIMU WAENDELEA SINGIDA


Fredrick Ndahani, Singida
Mgomo wa Walimu umezidi kuchukua kasi Mkoani Singida ambapo asilimia kubwa ya walimu katika Manispaa ya Singida, wameitikia mgomo huo licha ya serikali mkoani humo kutishia kuwafukuza kazi walimu waliogoma.
Mgomo huo umeendela katika shule za msingi kumi na moja ikiwamo shule ya msingi Ukombozi, Kibaoni, Mahembe, Ipembe, Sumaye, Singidani, Mughanga, Sabasaba, Utemini  Minga na Nyerere ambapo walimu wakuu ndio wameonekana kufika shuleni.
Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Ukombozi Samwel Kingu amesema wamelazimika kufika shuleni hapo kulinda mali za shule kwa kuwa wanahofia kuwepo kwa uharibifu wa mali hizo.
Naye Katibu wa CWT wa Mkoa Aran Jumbe amesisitiza walimu wote kuendelea kukaa majumbani mpaka tamko rasmi kutoka kwa Rais wa Chama hicho la kuendelea na kazi litakapotolewa.
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa