Home » » RC SINGIDA AAGIZA ZANAHATI IPEWE WAHUDUMU WENYE SIFA

RC SINGIDA AAGIZA ZANAHATI IPEWE WAHUDUMU WENYE SIFA

 
Na Nathaniel Limu, Singida
MKUU wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone, amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Iramba ashirikiane na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri kuhakikisha Zahanati ya Kitongoji cha Kipamba iliyopo Kata ya Mwangeza inakuwa na wahudumu wenye sifa mapema iwezekanavyo.

Agizo hilo lilitolewa mjini hapa juzi baada ya kulalamikiwa na wakazi wa Kitongoji cha Kipemba kwamba zahanati yao toka imalizike kujengwa zaidi ya mwaka moja haina muhudumu mwenye taaluma.

Imedaiwa kuwa kwa kipindi chote hicho, kuna vijana wawili wenye elimu ya msingi na ambao hawajasomea taaluma ya utoaji huduma ya afya ndio wanaotoa huduma.

“Haingii akilini zahanati ambayo imejengwa kwa msaada na Shirika la International Outreach Africa la nchini Marekani, imebaki bila mhudumu wa afya mwenye sifa stahiki. Wafadhili hawa wakija leo, hivi watatuelewaje,” alihoji Dk. Kone.

Kutokana na hali hiyo, aliagiza wahudumu wenye sifa stahiki, wapangwe haraka iwezekanavyo katika zahanati hiyo.

Kuhusu malalamiko ya ukosefu wa vitanda katika mabweni mawili ya Shule ya Msingi ya Munguli, aliagiza taratibu zifanywe haraka na hatimaye mabweni hayo yawe na vitanda vyitakavyokidhi mahitaji.

Baadhi ya wakazi wa Kitongoji cha Kipamba, wamedai kero zao nyingi hazipatiwi ufumbuzi wa kudumu kwa madai Mbunge wao, Salome Mwabu, hajawatembelea toka amechaguliwa kushika wadhifa huo.
Chanzo: Mtanzania

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa