Home » » BEI YA VYAKULA VYA FUTARI YAPANDA MARA MBILI SINGIDA

BEI YA VYAKULA VYA FUTARI YAPANDA MARA MBILI SINGIDA


Fredrick Ndahani
BEI ya vyakula katika Manispaa ya Singida imepanda mara dufu katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani ambapo bei ya maboga imepanda toka sh.500 hadi kufikia kati ya sh.1,000 na 2,000 kwa boga moja.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi umebaini kupanda kwa bei ya viazi, maboga, na bidhaa nyingine ambazo na kuwakazwa wakazi wa mjini hapa.
Mmoja wa wauzaji wa bidhaa hizo katika soko la Marunda na Mboga mboga Deus Mwijage alisema kuwa wamelazimika kupandisha bei ya maboga kutoka na kukosekana kwa mihogo ambayo ilikuwa inasaidia wakati wa mwezi wa ramadhani.
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa