Home » » NYAMAPORI KUTUMIKA KUIHAMASISHA JAMII YA WAHADZABE KUSHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI.

NYAMAPORI KUTUMIKA KUIHAMASISHA JAMII YA WAHADZABE KUSHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI.

Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt.Parseko Kone (mwenye suti ya bluu) akisalimiana na mzee wa Kihadzabe mkazi wa kijiji cha Munguli kitongoji cha Kipamba ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja.
Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone akihamasisha jamii ya Kihadzabe wa kitongoji cha Kipamba kushiriki sensa ya taifa inayotarajiwa kufanyika nchini kote Agosti 26 mwaka huu.
Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone (mwenye suti ya bluu)akimkabidhi msaada wa chakula Mwenyekiti wa kitongoji cha Kipamba kijiji cha Munguli Edward Mashimba (mwenye shati jeupe).
Maboksi ya msaada wa chakula kilichotolewa na shirika lisilo la kiserikali la International Outreach International na nchini Marekani. Chakula hicho kina uzito wa zaidi ya tani moja.
Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone, akiwa amempakata mtoto wa Kihadzabe aliyebatizwa jina lake la Kone. Mtoto huyo alizaliwa asubuhi ya siku Dkt. Kone alipofanya ziara ya kwanza ya kikazi katika kijiji hicho miaka sita iliyopita. Nyuma ya mtoto huy ni Mkuu wa wilaya ya Singida Mwalimu Queen Mlozi.
Baadhi ya akina mama wa Kihadazbe waliohudhuria mkutano wa hadhara ambao mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone, aliutumia kuhamasisha jamii ya Kihadzabe na nyingine kushiriki sensa inayaotarajiwa kufanyika Agosti 26 mwaka huu. (Picha zote na Nathaniel Limu).
Na.Nathaniel Limu.
Serikali ya wilaya mpya  ya Mkalama mkoani SIngida imeahidi kutoa nyama pori ya kutosha kwa Wahadzabe wa kitongoji cha Kipamba kata ya Mwangeza, ili waweze kushiriki sensa ya kitaifa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika nchini kote Agosti 26 mwaka huu.
Kwa mujibu wa mkuu wa wilaya hiyo Edward Ole Lenga, msaada wa nyama ya wanyama pori hiyo, utasaidia jamii ya Wahdzabe kubaki kwenye kaya zao kipindi chote cha sensa.
Akizungumza muda mfupi kabla ya kumkaribisha mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone, awahamasishe Wahadzabe na wakazi wengine wa kata ya Munguli, kushiriki sensa.
Lenga amesema msaada huo wa  nyama pori, unatokana na ombi liliotolewa na jamii hiyo ambayo chakula chake kikuu ni nyamapori, mizizi, matunda pori na asali.
Akifafanua amesema Wahdzabe hao wanaokadiriwa kufikia 227, wametoa ombi hilo ili wakati wote wa sensa wasiende porini kuwinda na badala yake wabaki kwenye kaya zao wakisubiri kuhesabiwa.
Mkuu huyo wa wilaya amesema ombi hilo tayari limeshakubaliwa na maandalizi yote muhimu ya kuwinda wanyama pori siku moja kabla ya siku ya sensa, yamekwisha kamilika.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa Dkt. Kone, ametoa msaada wa chakula chenye uzito wa zaidi ya tani moja, ambacho kitakidhi mahitaji kuanzia sasa hadi zoezi la sensa litakapokamilika.
Amesema kwa hali hiyo, kipindi chote cha sensa, hapatakuwepo na haja kwenda porini kutafuta wanyama pori, asali, matunda pori au mizizi.
Katika hatua nyingine, amewataka wahakikishe kila mmoja anahesabiwa mara moja tu, kwa madai kuwa wakishafahamika idadi yao na hali zao za maisha, itasaidia serikali kujipanga namna bora  ya kuwahudumia na kuwaletea maendeleo.
Wakati huo huo Dk. Kone, amesema pamoja na kunid la wawindaji, pia makundi mengine ya wavuvi, wachungaji wanaohama hama, watafutaji madini na baadhi ya wakulima ambao wana mashamba yaliyo mbali na makazi au makambi yao ya kawaida, warejee kwenye kaya na makambi yao ili waweze kuhesabiwa siku ya sensa.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa