Home » » WALIMU SINGIDA WATISHIA KUKWAMISHA ZOEZI LA SENSA

WALIMU SINGIDA WATISHIA KUKWAMISHA ZOEZI LA SENSA

Fredrick Ndahan, Singida Yetu
Baadhi ya walimu wa shule za sekondari na msingi katika Manispaa ya Singida wametishia kutoshiriki katika kutoa taarifa katika zoezi la sensa baada ya kutolewa katika orodha ya makalani na makalani wandamizi wakati wa zoezi hilo.
Wakiongea na mwandishi wa habari hizi katika maeneo tofauti tofauti wamesema hakuna haja ya kushiriki katika zoezi hilo kwani walioteuliwa hawana vigezo kama ilivyoanishwa katika tangazo la nafasi za kazi lilotolewa.
Walimu hao wamesema kuwa kunamawakala hawajamaliza elimu ya sekondari jambo ambalo linaweza kukwamisha zoezi hilo kwa kusimamiwa na watu wasio na sifa stahiki.
Akizungumza kwa masharti ya kutotajwa jina lake huku akionesha mitihani aliyofaulu baada ya zoezi la semina amesema nashangaa kuona jina lake na baadhi ya walimu wenzake licha kuchaguliwa kushiriki katika zoezi la sensa kama wakufunzi lakini wamewekwa maofisa wengine ambao hawakushiriki mafunzo ya awali ya zoezi la sensa.
Mbali na tatizo hilo pia kuna makalani wengine wamepangiwa kufanya shughuli hiyo katika maeneo ambayo si makazi yao kinyume cha utaratibu.
Manispaa ya Singida jana ilianza semina ya makalani wandamizi katika ukumbi wa chuo cha maendeleo singida (FDS).
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa