Home » » RC SINGIDA: WAELIMISHENI WANANCHI MATUMIZI BORA YA RASILIMALI

RC SINGIDA: WAELIMISHENI WANANCHI MATUMIZI BORA YA RASILIMALI


Na Emmanuel Michael, Singida

KAMATI za mikoa za baraza la ushauri la watumiaji wa huduma za nishati  na maji  nchini, zimetakiwa kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa matumizi bora ya raslimali hizo.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone wakati akizindua kamati hiyo.

Dk. Kone amesema licha ya kuwepo kwa changamoto ya uhaba wa nishati na maji na kupanda kwa bei zake, lakini baadhi ya watumiaji wa huduma hizo wamekuwa na matumizi mabaya.

Kutokana na hali  hiyo amesema  kuna  haja kwa kamati  za mikoa za ushauri wa baraza la watumiaji wa huduma za nishati na maji  kutoa elimu kwa wananchi  juu ya  kutunza na kutumia vyema raslimali hizo.


Amesema hatua hiyo itasaidia katika kuhakikisha kuwa nishati kidogo na maji yanayopatikana yanatumika kwa uangalifu ili kukidhi mahitaji na kupunguza malalamiko ya kupanda bei.

Kamati  hiyo yenye wajumbe sita imeundwa kwa mujibu wa sheria  ya  mamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji (EWURA) kifungu cha 30, ikiwa na  jukumu la kusimamia maslahi ya watumiaji wa huduma hizo na kushauriana na wenye viwanda na wadau wengine.

Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa