Home » » MTENDAJI WA KIJIJI AFUNGWA KWA KUOMBA RUSHWA

MTENDAJI WA KIJIJI AFUNGWA KWA KUOMBA RUSHWA

 
Na Petro Sungi, Singida
AFISA mtendaji wa Kijiji cha Misuke kilichopo katika Wilaya ya Singida, Omary Mandi amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu, baada ya kukutwa na hatia ya kuomba na kupokea rushwa.

Hukumu hiyo ilitolewa Agosti 21, mwaka huu na Hakimu Mkazi wa Mahakama mkoani hapa, Ruth Massam mbele ya Ofisa Uchunguzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa mkoani hapa (TAKUKURU), Wilson Ntiro.

Katika hukumu hiyo mtuhumiwa alikutwa na hatia ya kuomba na kupokea rushwa mara mbili na kuhukumiwa kwenda jela miaka mitatu.

Awali Ofisa wa TAKUKURU alidai kuwa mtuhumiwa huyo alitenda makosa hayo Novemba 17, 2010 kwa kupokea rushwa ya Sh 40, 000 wakati Novemba 10 alipokea rushwa ya Sh 75, 000 kutoka kwa Mwenyekiti wa Misuke, Joseph Dwash.

Mtendaji huyo alidaiwa kuwa alimdanganya Dwash kuwa anaweza kumsaidia, ili aendelee kuwa mwenyekiti. Kesi hiyo ilifunguliwa Januari 31, mwaka huu na TAKUKURU.
Chanzo: Mtanzania

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa