Home » » 38 WACHUANA UVCCM SINGIDA

38 WACHUANA UVCCM SINGIDA

 
Na Nathaniel Limu, Singida
JUMLA ya wanachama 38 wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) mkoani Singida, wamejitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa jumuiya hiyo, unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Katibu wa UVCCM Singida, Omary Mtua, aliwataja Dinya Shabani Hamisi, Hamisi Haji Nkuwei, Heri Shaaban Kundya, Labia Martin Zephania, Prince Antonio na Rehema Omari Sombi wanaogombea nafasi ya mwenyekiti wa UVCCM mkoa.

Alisema kwa upande wa nafasi ya mwenyekiti Singida mjini, nafasi hiyo imeombwa na Fikirini Hassan Salim, Yassin Mdima, Ibrahimu Alli na Shaaban Mhimbani.

Aidha, Mtua aliwataja Elia Sidadi, Shaaban Mangola, Madiu Ndwete na Yohana Mnyangili kuwa wameomba nafasi ya uenyekiti wilaya ya Singida vijijini.

“Kwa upande wa wilaya mpya ya Ikungi, nafasi ya mwenyekiti wa UVCCM imeombwa na Rebein Elisha Ibrahim (Anatetea nafasi yake), John Mughenyi, Joramu Ntandu, Yona Mwangu, Norman Mkola na Rajabu Njoha,” alisema katibu huyo.

Alisema nafasi ya mwenyekiti UVCCM wilaya ya Manyoni, imeombwa na Omari Miraji, Faraji Idd, Emmanuel Chitambi, Anjelo Madundoo na Jane Likuda.

Aidha aliwataja Belinda Matalu, Juliana Zingula, Mary Mkoma, Muungano Senyagwa na Athumani Rajabu ambao wameomba nafasi ya Mwenyekiti wa wilaya ya Iramba.

“Nafasi ya mwenyekiti UVCCM wilaya ya Mkalama, imeombwa na Hamidu Omari, Jofiliki Mkwega, Joseph Saeda, Kiula Solomon na Sebastian Gunda,” alisema Mtua.

Wakati huo huo, Mtua aliwataja Dinya Hamisi, Hansi Nkuwi, Prince Antonio na Sabasaba Manase ambao wameomba nafasi ya mjumbe wa NEC kupitia tiketi ya mkoa wa Singida kutoka UVCCM.

Alisema nafasi ya mjumbe wa baraza kuu taifa mkoa wa Singida, imeombwa na Heri Kundya, Dinya Hamisi, Joel Missanga, Jamila Kitila, Mazaba Warioba, Prince Antonio na Sabasaba Manase.
Chanzo: Mtanzania

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa