Home » » Wanahabari Watakiwa Kufuata Maadili Ya Uandishi Kuepuka Migogoro

Wanahabari Watakiwa Kufuata Maadili Ya Uandishi Kuepuka Migogoro




MWENYEKIT wa Klabu ya wanahabari mkoa Singida SINGPRESS) Seif Takaza akizungumza kabla ya kumkaribisha Yahaya Nawanda, mkuu wa wilaya ya Iramba kufungua mkutano maalum wa kufanyia marekebesho KATIBA ya klabu hiyo(kushoto ni kuu huyo wa Wilaya).
Mkuu wa Wilaya ya Iramba Yahaya Nawanda, akifungua mkutano maalum wa klabu ya waandishi wa habari Mkoa Singida(Singpress) ulioandaliwa kwa ajili ya kuifanyia marekebisho katiba ya klabu,kuanzia kulia ni makamu Mwenyekiti wa Singpress, Jumbe Ismaely, anayefuata ni mwenyekiti wa Singpress Seif Takaza.



Mkuu wa wilaya Iramba Yahaya Nawanda (wa pili kulia - mwenye miwani),akiwa katika picha ya pamoja na wanahabari wa mkoa Singida, muda mfupi baada ya kufungua mkutano maalumu wa Katiba ya Singpress.





Na: Elisante John, Singida



Mkuu wa Wilaya Iramba Mkoani Singida, Yahaya Nawanda, ametoa wito huo alipofungua mkutano mkutano maalumu wa Katiba ya Klabu ya wanahabari mkoa Singida (SINGPRESS), uliofanyika ukumbi wa halmashauri, mjini Kiomboi.



Alisema kuna faida nyingi kwa kutii na kuzingatia katiba watakayoifanyia marekebesho, mojawapo ikiwa ni kuimarisha amani na utulivu ndani ya kikundi, nchi au sehemu yoyote ile kwa watu walioamua kushirikiana pamoja.




Pia alihimiza wanahabari hao waende sawa na mabadiliko yatakayofanyika ili kujenga umoja na upendo miongoni mwao na wadau wengine wa habari Mkoani Singida.




Aliwataka wasiingize ushabiki katika utendaji wao wa kazi za kila siku, kuepusha tasnia ya habari kuonekana kazi isiyofaa katika jamii.


0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa