Mwandishi wetu, Singida Yetu 
SERIKALI imewataka watu waliovamia pori wanaloishi wananchi wa kabila la wahadzabe mkoani Singida kuondoka mara moja kabla hatua za kisheria hazijachukuliwa dhidi yao.
Pori  hilo lililopo katika Kijiji  cha Munguli wilaya  Mkalama umbali wa kilomita 120  kaskazini mashariki mwa mji wa Singida, limevamiwa na wahamiaji  kutoka Arusha, Manyara na  Shinyanga  ambao wamefyeka na kuchoma  moto kwa ajili ya  kilimo na ufugaji.
Akizungumza  baada ya kuwatembelea wananchi  hao  maarufu kama watindiga Mkuu wa Mkoa wa Singida Dokta Parseko Kone amesema serikali haiwezi kuvumilia  kuona uharibifu wa mazingira ukiendelea katika pori hilo lililotengwa na kuhifadhiwa kwa mujibu wa sheria.
Dokta Kone amemwagiza mkuu wa wilaya ya Mkalama na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, kuwaondoa wavamizi hao kwa nguvu iwapo hawataondoka kwa hiari yao.
Mbali na wavamizi, pori hilo linakaliwa na wahadzabe zaidi 400  ambao hujishughulisha na  uwindaji na kula vyakula  vya  asili ambavyo ni nyama pori, asali, matunda pori na mizizi
Blogzamikoa
0 comments:
Post a Comment