Home » » WAZIRI NYARANDU KUCHMBA KISIMA SINGIDA

WAZIRI NYARANDU KUCHMBA KISIMA SINGIDA

Na Emmanuel Michael, Singida
WAKAZI wa kijiji cha Mnung’una jimbo la Singida kaskazini  pamoja na maeneo jirani hivi karibuni  wanatarajia kuondokana na tatizo la ukosefu wa maji safi na salama lililokuwa linawakabili kwa miaka mingi.

Matumaini ya kumalizika kwa tatizo  hilo yamekuja baada ya mbunge wa jimbo hilo Mhe Lazaro Nyalandu  kufadhili uchimbaji wa kisima kirefu kwa gharama ya shilingi milioni 25 katika eneo hilo.
Mbunge Nyalandu amesema kukamilika kwa kisima hicho kilichoanza kuchimbwa jana kutaondoa adha kwa wananchi kutembea umbali mrefu na kupoteza muda wa kufanya shughuli za maendeleo kwa kutafuta maji.
Amesema kisima hicho kinachotarajiwa kuwa na uwezo wa kuzalisha lita 10,000 za maji  kwa saa moja ni sehemu ya  utekelezaji kwa  vitendo  sera ya taifa  ya maji inayotaka huduma hiyo kupatikana  umbali usiozidi mita 400 kutoka makazi ya watu.
Baada ya kukamilika kwa uchimbaji wa kisima  hicho, mradi huo unatarajia kuwanufaisha zaidi ya wananchi elfu saba kwa kujipatia  huduma maji  safi na salam kwa ajili ya matumizi ya nyumbani, kunywesha mifugo yao na  kuendesha  kilimo cha bustani.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa